Connect with us

News

EACC: Wizara ya Usalama na Afya zaongoza kwa ufisadi

Published

on

Utafiti mpya wa kitaifa uliofanywa na Tume ya maadili ya kupambana na ufisadi nchini EACC umeonya wakenya dhidi ya vitendo visivyo vya kimaadili na ufisadi katika Wizara ya usalama wa ndani na taasisi nyingine za umma.

Kulingana na utafiti wa mwaka 2024 wa tume hiyo, asilimia 47.8 ya wakenya waliotangamana na Wizara ya usalama wa ndani waliripoti kupitia au kushuhudia vitendo vya ufisadi au visivyo vya kimaadili.

Hali hii inaifanya Wizara hiyo kuwa na kiwango kikubwa cha matukio kama haya.

Wizara ya Afya nchini ilishika nafasi ya pili kwa asilimia 19.7, huku hazina ya kitaifa ikifuata kwa mbali kwa asilimia 5.8.

Taasisi nyingine za umma zilizojitokeza kwa wingi ni pamoja na wizara ya Ardhi kwa asilimia 5.6, uchukuzi kwa asilimia 3.9, na elimu kwa asilimia 2.6.

Utafiti huo uliofanywa kati ya Agosti na Oktoba 2024, uliwashirikisha zaidi ya watu 6,000 kote nchini na ulilenga kuelewa mitazamo na uzoefu wa wananchi kuhusiana na rushwa na maadili katika utumishi wa umma.

Ripoti hiyo ilifichua kuwa wakenya bado wanakabiliana na viwango vya juu vya hongo na tabia isiyofaa katika taasisi za umma.

Pia ilifichua hali inayotia wasiwasi ambapo rushwa inazidi kuonekana kama uovu muhimu katika kupata huduma za umma.

Ripoti hiyo pia ilibainisha kuwa wananchi wengi wanahisi wamenaswa katika mzunguko wa unyang’anyi na kuogopa kudhulumiwa ikiwa watazungumza.

Kaunti ya Nairobi iliongoza orodha ya vitengo vya ugatuzi ambapo wakaazi waliripoti kukabiliwa na visa vya juu zaidi vya ufisadi, ikifuatiwa na Kiambu, Machakos, Kisumu na Nakuru.

Tume hiyo iliwataka watumishi wa umma kuzingatia maadili ya uadilifu, uwazi na uwajibikaji katika kutoa huduma kwa Wakenya.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending