News
Familia ya Kenyatta yatoa milioni 1.5 kusaidia Kanisa Katoliki Watamu
Familia ya rais mstaafu Uhuru Kenyatta imetoa shilingi milioni 1.5 kusaidia ujenzi wa kituo cha uchungaji cha Stella Maris Pastoral Center katika eneo la Watamu katika kaunti ya Kilifi.
Rais mstaafu Kenyatta alikuwa ameandamana na mkewe Bi Margaret Kenyatta pamoja na familia yao akiwemo Maina Gakuo na mkewe Anna Kadzo Gakuo Kenyatta, walipokelewa na Askofu wa Kanisa Katoliki jimbo la Malindi Willybard Lagho.
Kenyatta alilipongeza jimbo Katoliki la Malindi kwa kujitolea kujiimarisha kifedha kupitia mradi huo na kwamba aliahidi kulisaidia jimbo hilo hadi kituo hicho cha kichungaji kitakapokamilika.

Rais mstaafu Uhuru Kenyatta, Bi Margaret Kenyatta, Askofu wa Malindi Willybard Lagho pamoja na mapadre na familia ya Kenyatta katika kituo cha Stella Maris, Watamu {picha kwa hisani}
Naye Askofu mkuu wa Kanisa Katoliki jimbo la Malindi Willybard Lagho, alishukuru msaada huo kutoka kwa familia ya rais mstaafu Uhuru Kenyatta kwa niaba ya Jumuiya ya Kikatoliki huku akipongeza juhudi za Mapadre wa jimbo hilo la Malindi katika kufanikisha uendelezi wa ujenzi wa kituo hicho hasa Padre Bernard Malasi, Padre Stephen Kadenge na Padre David Ndwiga.
Askofu Lagho, hata hivyo aliishukuru familia ya Kenyatta kwa ukarimu wao na kuwahakikishia kwamba dayosisi ya Malindi itawapa taarifa zaidi kuhusu maendeleo ya ujenzi wa kituo hicho cha kichungaji.
Kituo hicho cha kichungaji cha Stella Maris kinatarajiwa kutumika kama kitovu cha kiroho, kijamii na kiuchumi kwa jumuiya ya kikatoliki na Jimbo kuu la Malindi mara kitakapokamilika.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

