Connect with us

International News

Tume ya uchaguzi ya Tanzania INEC yazima ndoto ya Luhaga Mpina

Published

on

Tume huru ya uchaguzi nchini Tanzania (INEC) imekiandikia chama cha upinzani cha ACT Wazalendo kuwa hakitaweza kumteua mgombea wa urais kupitia chama hicho, Luhaga Mpina.

Katika barua ambayo INEC imeiandikia ACT-Wazalendo, tume hiyo ya uchaguzi ilirejea uamuzi wa Ofisi ya msajili wa vyama vya siasa uliotolewa siku ya Jumatano Agosti 27, 2025 ambao ulisema mgombea wa urais wa chama hicho Luhaga Mpina, hakukidhi matakwa ya Katiba na kanuni za ACT kuwania nafasi hiyo.

ACT-Wazalendo walipokea barau kutoka kwa msajili wa vyama vya kisiasa kujieleza jinsi ilivyoendesha mchakato wa kumpata mgombea wake wa urais kama yalivyokuwa madai ya mwanachama wa chama hicho, Manalisa Ndala.

Barua hiyo ya INEC ilihitimisha kwa kueleza kwamba inafuta barua yake ya Agosti 15,2025 kuhusu urejeshaji wa fomu kwa mgombea na kumtaka asifike katika ofisi hizo kwa ajili ya uteuzi.

Hata hivyo, chama cha ACT-Wazalendo kilisema kwenye taarifa yake kwamba kinaupinga uamuzi wa Ofisi ya majili na pia kilisema Tume ya uchaguzi ilijiongoza vibaya kwenye kukubaliana na kile uchaguzi mkuu Tanzania kufanyika Oktoba 29.

Chama cha ACT- Wazalenzo kilishikilia kwamba maagizo ya msajili mkuu wa vyama vya kisiasa ni kinyume na matakwa ya kikatiba yanayoitangaza Tume hiyo kuwa ni huru na isiyochukuwa amri kutoka chombo chochote kile.

Katika taarifa hiyo, Katibu mkuu wa chama hicho, Ado Shaibu, aliiomba Tume ya Uchaguzi kubadilisha uamuzi wake na kutokuifanya ionekane kutokuwa huru kwenye utekelezaji wa kazi zake kisheria.

Hata hivyo mgombea wa urais wa chama cha CCM, Samia Suluhu Hassan na chama cha upinzani cha NRA, Hassan Kisabya Almas, walikamilisha hatua ya uteuzi na kukabidhiwa magari aina ya Landcruiser ambayo watayatumia katika kampeni zao za uchaguzi zinazotarajia kuzinduliwa.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

International News

Vita dhidi ya Al-Shabab vya shika kasi Somalia

Published

on

By

Operesheni kali ya kijeshi inayoendelea nchini Somalia ambapo zaidi ya wanamgambo 33 wa kundi la Alshabab wameuawa katika eneo la Shabelle nyanda za chini za Jubaland.

Ufanisi wa operasheni hii ya hivi punde ni muendelezo wa oparesheni iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Aprili 24 katika eneo hilo la Juba ambapo Wanamgambo 27 wa AlShabab waliuawa.

Hii ina maana kwamba Jeshi la Somali limefanikiwa kuvunja maficho muhimu ya kundi hilo, ambalo kufikia sasa ya Wanamgambo 60 wameuawa

Kwa mujibu wa vianzo vya habari hususan kutoka kwa maafisa wa usalama, operesheni hiyo inafanyika kufuatia taarifa za kijasusi kuhusu maficho ya wanamgambo hao waliokuwa wakipanga mashambulizi dhidi ya vituo muhimu na taasisi za serikali.

Wanajeshi hao walivamia ngome za magaidi hao kwa ustadi mkubwa, wakifanikiwa kudhibiti eneo hilo baada ya mapambano makali yaliyochukua muda wa saa kadhaa.

Maafisa wamesema kuwa mafanikio hayo ni sehemu ya juhudi zinazoendelea za kuimarisha usalama na kuangamiza kabisa mtandao wa Al-Shabaab ambao kwa muda mrefu umekuwa ukihatarisha amani katika maeneo mbalimbali ya Somalia na ukanda mzima wa Afrika Mashariki.

Wananchi wa eneo la Jubbaland wameelezea matumaini mapya kufuatia operesheni hiyo, wakisema kuwa hatua hiyo inaleta nuru ya kurejea kwa utulivu na maendeleo baada ya miaka ya hofu na mashambulizi ya mara kwa mara nchini.

Serikali imeapa kuendeleza msako dhidi ya wanamgambo hao hadi pale watakapokomesha kabisa vitisho vya mashambulio , huku ikiwataka wananchi kushirikiana na vyombo vya usalama kwa kutoa taarifa zitakazosaidia kudhibiti ugaidi.

Taarifa ya Billy Mongo

Continue Reading

International News

Kumbukumbu za muaji ya kimbari Rwanda

Published

on

By

Ni miaka 32 tangu kutokea kwa mauaji ya kimbari nchini Rwanda.

Leo, tarehe saba Aprili, raia wa Rwanda pamoja na dunia kwa ujumla wanaungana kukumbuka kuanza kwa mauaji ya kimbari ya mwaka 1994, ambapo zaidi ya watu laki nane, wengi wao wakiwa jamii ya Watutsi, waliuawa ndani ya kipindi cha siku mia moja.

Tarehe hii ni ya kihistoria kwa taifa hilo ambalo miaka 32 iliyopita lilikumbwa na moja ya matukio ya kikatili zaidi katika historia ya mwanadamu.

Mauaji hayo yalichochewa na kuuawa kwa aliyekuwa rais wa Rwanda Juvenal Habyarimana, tukio lililosababisha kuzuka kwa vurugu kote nchini.

Kilichofuatia ni mashambulizi ya kimbari kati ya Wahutu na Watutsi, ambapo zaidi ya watu milioni moja wanaripotiwa kupoteza maisha katika muda wa siku mia moja.

Wanawake, wanaume na watoto walilengwa katika mashambulizi hayo yaliyopangwa, jamii zikivunjika na dunia ikishuhudia tukio hilo kwa muda bila kuchukua hatua za haraka kuzuia maafa hayo.

Katika kuadhimisha siku hii, inayojulikana kama KWIBUKA, yenye maana ya “tunakumbuka,” bendera nchini Rwanda zinapepea nusu mlingoti, huku Rais Paul Kagame akitarajiwa kuwasha mwenge wa kumbukumbu katika makavazi ya Kigali.

Hata hivyo, licha ya historia hiyo ya maumivu, Rwanda imepiga hatua kubwa katika kipindi cha miongo mitatu iliyopita, ikijijenga upya kutoka jamii iliyogawanyika hadi kuwa taifa lenye umoja, likishuhudia maendeleo ya kijamii na kiuchumi pamoja na juhudi za maridhiano na haki kwa wahanga.

Leo hii, Rwanda inasimama kama mfano kwa mataifa mengine aduniani, huku wito wa kuhakikisha mauaji ya kimbari hayajirudii tena ukiendelea kusisitizwa.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

Trending