News
Familia yalilia haki baada ya mtoto wao kufariki baada ya kupigwa kichwa na mwalimu
Familia moja eneo la Junju kaunti ya Kilifi inalilia haki baada mtoto wao kwa jina Anestine Dzidza Tunje mwanafunzi mwenye umri wa miaka 15 wa Gredi ya 8 katika shule ya Msingi ya Gongoni iliyoko Junju anayedaiwa kupigwa na mwalimu hadi kuvuja damu ndani ya kichwa chake hali iliyomfanya kufariki.
Akizungumza na waandishi wa habari nje ya hospitali ya rufaa mjini Kilifi kaunti ya Kilifi, Alex Tunje Mzungu alisema kuwa mwanawe alianza kusema ana maumivu kwenye mwili wake hali iliyomfanya kupeleka hospitalini ili kupata huduma za matibabu katika hospitali ya Vipingo.
Mzungu alisema kuwa mwanawe alizidiwa na ndipo alipochukua hatua ya kumpeleka pia katika hospitali ya rufaa mjini Kilifi ambapo alilazwa na kisha kufariki na kulingana na ripoti ya upasuaji kutoka kwa daktari marehemu alifariki kutokana na hali ya kuvuja damu ndani ya kichwa chake.
“Nikamuuliza vipi waendeleaje akisema anaskia vibaya nikamchukua nikampeleka hospitali’’ alisema Mzungu
Kwa upande wake Jimmy Thoya na Caroline Mbeyu ambao pia ni wanafamilia waliitaka idara ya usalama kumchukulia hatua za kisheria mwalimu huyo na pia kuweka mikakati ambayo itadhibiti visa kama hivyo kutokea shuleni.
Kwa upande wake Salome Karisa ambaye ni mtetezi wa haki za watoto alikashifu kitendo hicho na kuahidi kama mashirika ya kutetea haki za kibinadamu watahakikisha haki inapatikana kwa familia hiyo.
“Tunapinga vikali kitendo kama hiki ya uvunjaji wa sheria hususan kwa haki za watoto na tunaomba yule mwalimu aliyehusika apate kuchukuliwa hatua’’ alisema Karisa
Taarifa ya Janet Mumbi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

