News
Mahakama ya Kilifi yamnyima dhamana mshukiwa wa unajisi
Mahakama ya Kilifi imemnyima dhamana mwanaume mmoja anayekabiliwa na shtaka la unajisi wa mtoto wa umri wa miaka 11 kisha kutishia kumuua iwapo angesema kuhusu kitendo hicho.
Hakimu wa Mahakama hiyo Ivy Wasike aliagiza kuzuiliwa rumande kwa mshukiwa huyo Hamis Bakari Karisa baada ya kiongozi wa mashtaka Nancy Njeru kueleza Mahakama kwamba mshukiwa huyo ana kesi yengine ya kujibu ya unajisi katika Mahakama hiyo iliyowasilishwa mbele ya Hakimu Charles Obulutsa.
Vile vile kiongozi wa mashtaka alieleza Mahakama kwamba mshukiwa alitekeleza kitendo hicho cha unajisi baada ya kuachiliwa kwa dhamana kwa kesi awali aliyokuwa ikimkabili ya unajisi ambayo bado inaendelea.
Awali Mahakama ilielezwa kwamba mshtakiwa alitekeleza kitendo hicho cha unyama siku tofauti kati ya tarehe 23 hadi 29 mwezi Septemba mwaka 2025 eneo la Tezo kaunti ya Kilifi.
Hata hivyo Mahakama iliagiza mshukiwa kurudishwa Mahakamani mnamo tarehe 20 mwezi Novemba mwaka 2025 ambapo kesi hiyo itasikizwa mbele ya Hakimu James Mwaniki
Taarifa ya Teclar Yeri
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

