Connect with us

News

Familia yalilia haki baada ya mtoto wao kufariki baada ya kupigwa kichwa na mwalimu

Published

on

Familia moja eneo la Junju kaunti ya Kilifi inalilia haki baada mtoto wao kwa jina Anestine Dzidza Tunje mwanafunzi mwenye umri wa miaka 15 wa Gredi ya 8 katika shule ya Msingi ya Gongoni iliyoko Junju anayedaiwa kupigwa na mwalimu hadi kuvuja damu ndani ya kichwa chake hali iliyomfanya kufariki.

Akizungumza na waandishi wa habari nje ya hospitali ya rufaa mjini Kilifi kaunti ya Kilifi, Alex Tunje Mzungu alisema kuwa mwanawe alianza kusema ana maumivu kwenye mwili wake hali iliyomfanya kupeleka hospitalini ili kupata huduma za matibabu katika hospitali ya Vipingo.

Mzungu alisema kuwa mwanawe alizidiwa na ndipo alipochukua hatua ya kumpeleka pia katika hospitali ya rufaa mjini Kilifi ambapo alilazwa na kisha kufariki na kulingana na ripoti ya upasuaji kutoka kwa daktari marehemu alifariki kutokana na hali ya kuvuja damu ndani ya kichwa chake.

“Nikamuuliza vipi waendeleaje akisema anaskia vibaya nikamchukua nikampeleka hospitali’’ alisema Mzungu

Kwa upande wake Jimmy Thoya na Caroline Mbeyu ambao pia ni wanafamilia waliitaka idara ya usalama kumchukulia hatua za kisheria mwalimu huyo na pia kuweka mikakati ambayo itadhibiti visa kama hivyo kutokea shuleni.

Kwa upande wake Salome Karisa ambaye ni mtetezi wa haki za watoto alikashifu kitendo hicho na kuahidi kama mashirika ya kutetea haki za kibinadamu watahakikisha haki inapatikana kwa familia hiyo.

“Tunapinga vikali kitendo kama hiki ya uvunjaji wa sheria hususan kwa haki za watoto na tunaomba yule mwalimu aliyehusika apate kuchukuliwa hatua’’ alisema Karisa

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending