Connect with us

News

FIDA yakemea unyanyasaji wa kimtandao kwa wanawake

Published

on

Shirika la wanawake mawakili nchini (FIDA) limekemea vikali ongezeko la visa vya dhulma za wanawake kwenye mitandao ya kijamii.

Mkurugenzi mtendaji wa shirika hilo Anne Ireri alidai ripoti nyingi zilizotolewa tangu mwaka 2022 zilionyesha kuwa wanawake wengi wamepitia dhulma za kimtandao.

Akizungumza wakati wa kuadhimisha miaka 40 ya shirika hilo katika eneo la Diani kaunti ya Kwale, Ireri aliitaka serikali ya kitaifa kuhakikisha haki za wanawake zinalindwa kupitia uundaji wa sheria dhabiti.

“Fida imetoa ripoti nyingi sana kuhusu unyanyasaji wa kimtandao ukiangalia ile ripoti yetu ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2022, na zaidi ya hapo tumekuwa mstarti wa mbele kuhimiza haswa serikali kuu kupitia waziri wa maswala ya mawasiliano na jinsia, tuwe na sheria dhabiti ili vile ambavyo tumesikia ukiwa na shida na mimi usiende mtandaoni kunivua nguo, kuna njia ya kuweza kufuata haki zako”, alisema Ireri.

Ni kauli iliyoungwa mkono na gavana wa Kaunti hiyo Fatuma Achani aliyewataka watumizi wa mitandao kuzingatia sheria zilizowekwa na serikali.

Vil;e vile gavana Achani aliwaonya wakaazi wa Kwale dhidi ya kutumia vibaya mtandao na kuwasilisha malalamishi yao kwa taasisi za uchunguzi.

“Hii ukiipendelea itakuja pia kudhuru familia yako, naona ni kitu ambacho tunafaa kukisimamisha, kama uko na malalamishi ofisi yangu iko wazi, mtu ambaye anamalalamishi anafaa kufika ofisini ili tunatatua hilo tatizo”,alisema gavana Achani.

Taarifa ya Mwanahabari

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending