Connect with us

News

Fikirini Jacobs: Serikali kuimarisha vijana kibiashara

Published

on

Katibu katika idara ya vijana na uchumi bunifu nchini Fikirini Jacobs amesema serikali imeweka mikakati kabambe ya kubuni ajira kwa vijana kupitia miradi ya kibiashara.

Akizungumza na Coco Fm, Jacobs alisema vijana ambao hawakamilisha elimu ya sekondari, wameangaziwa katika mradi wa kibiashara uitwao Nyota ambao serikali imeekeza pesa za kutosha.

Jacobs amedokeza kuwa mpango huo unaolenga vijana 100,000 utazinduliwa hivi karibuni nchini na vijana 70 katika kila wadi nchini watafaidi.

Alidokeza kuwa tayari idadi kubwa ya vijana wametuma maombi ya kusajiliwa katika mpango huo.

“Sehemu ya kwanza kutegemea na vile ambavyo zilitangazwa inaitwa Business Support, ni sehemu ambayo mhesimiwa rais alitangaza hata akiwa siku ya madaraka kule Homabay kwamba kumewekwa shilingi bilioni tano kati ya hizi bilioni zote ambazo lengo lake ni kuenda kusaidia vijana laki moja ambao ni vijana 70 kwa kila wadi ya Kenya”, alisema Fikirini

Pia alisema kuwa vijana wanaoishi na ulemavu nchini wamezingatiwa katika mpango huo katika juhudi za kuafikia usawa.

Vile vile alisema serikali imejenga vituo 155 vya kuwezesha kiujuzi vijana katika maeneo bunge yote nchini akidokeza kuwa kaunti ya Kilifi kuna vituo viwili zaidi ambavyo vitajengwa.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending