News
IEBC kufafanua mda mwafaka wa kampeni za uchaguzi
Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC Erastus Ethekon ametangaza mipango ya kushauriana na mwanasheria mkuu wa serikali ya Kenya ili kufafanua kipi kinajumuisha kampeni ya mapema kabla ya Uchaguzi mkuu wa 2027.
Akizungumza jijini Nairobi, Ethekon alisema Tume ya IEBC ina nia ya kufafanua mda wa kampeni na kuangazia masuala kuhusu utayarishaji wa uchaguzi kabla ya wakati.
“Nchini Kenya, kila siku, kila saa inafanana na msimu wa kampeni. Iwapo mtu atahudhuria hafla ya mazishi anazungumzia uchaguzi, hivyo inamaanisha ni kampeni? aliuliza Ethekon.
Mwenyekiti huyo mpya wa IEBC alisema ni vigumu kuangazia mda mwafaka wa kampeni ya uchaguzi unapofaa kuanza.
Kuhusu suala la uchaguzi ndogo nchini, Ethekon alihakikishia wakenya kwamba ratiba kamili itatolewa mara tu michakato ya ndani ya tume hiyo itakapokamilika.
“Kuhusu suala la muda wa uchaguzi mdogo, tutakuwa tukitangaza ratiba mara baada ya kamati ya uendeshaji kutoa taarifa zote kisha tutawasilisha maelezo. Kuweni na subira tutashughulikia ratiba,” alisema Mwenyekiti huyo.
Vile vile alikiri changamoto za kiutendaji zinazokabili tume hiyo japo akahakikishia wakenya kuwa hatua zinachukuliwa ili kuzitatua.
“Kulikuwa na baadhi ya mambo ambayo tuko nje ya udhibiti wetu, lakini tunafanya kazi usiku kucha kutekeleza shughuli hizi zote kama wale ambao wamepewa jukumu la kusimamia uchaguzi,” aliongeza Ethekon.
Hapo awali, Ethekon alisema uchaguzi mkuu wa 2027 utakuwa huru na wa haki, na kuondoa uwezekano wa wizi wa kura.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

