Connect with us

News

Gachagua: Upinzani hauna nia ya kupindua serikali

Published

on

Aliyekuwa naibu wa rais Rigathi Gachagua amekanusha madai kwamba mrengo wa upinzani unapanga kumuondoa rais William Samoei Ruto madarakani.

Katika taarifa yake ya siku ya Jumatano terehe 9 mwezi Julai, 2025 kwa vyombo vya habari, muda mfupi baada ya hotuba ya rais Ruto, Gachagua alisema vuguvugu la ONE TAM halina nia ya kuchukua mamlaka kwa njia ambayo sio halali.

Gachagua alimtaka rais Ruto kutekeleza majukumu yake ipasavyo na pia kudhibiti visa vya vya watu kutekwa nyara na kuuliwa katika mazingira tatanisha.

Gachagua pia alimkosoa rais Ruto akisema amekuwa akipuuza kilio cha wananchi hali ambayo inawafanya Wakenya wengi kuendelea kuhangaika.

‘’Bwana Ruto punguza hasira na kwa unyenyekevu mwingi nakushauri kwamba hasira sio suluhu maana haitakusaidia. Unapaswa kujua nini unapaswa kufanya maana haujakuwa ukiwasikiza Wakenya’’ alisema Gachagua.

Wakati huo huo, Gachagua ambaye pia ni Kinara wa chama cha DCP aliibua madai kwamba Rais Ruto amekuwa akiwatumia wahalifu kuharibu mali ya watu wakati maandamano ya vijana wa kizazi cha Gen Z ambao wamekuwa wakiandamana nchini kuwasilisha matakwa yao kwa serikali.

‘’Siku ya Sabasaba wahalifu hao walipeleka maandamano maeneo mbalimbali nchini hasa eneo la Mlima Kenya na yale mengine ambayo yanakashifu uongozi wa serikali kuu’’ aliongeza Gachagua.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending