News
Gachagua amtaka Rais Ruto kuangazia usalama wa Mandera
Kinara wa chama cha DCP Rigathi Gachagua amekosoa serikali kwa kusalia kimya kuhusiana na madai ya uwepo wa jeshi la Jubaland hapa nchini.
Naibu huyo wa rais wa zamani sasa anamtaka rais William Ruto kutoa amri ya kufurusha jeshi hilo kutoka eneo la Mandera na kurejesha hali ya usalama.
Akizungumza katika ibada ya jumapili katika kanisa la PCEA Ongata Rongai, Agosti 31, 2025, Gachagua alikashifu uvamizi huo akisema uwepo wa jeshi hilo utasambaratisha usalama mjini humo.
Vile vile alimlaumu rais Ruto akisema anachukua mda kukabiliana na ufisadi nchini suala ambalo linaendelea kurejesha nyuma maendeleo ya taifa.
“Nakusema wabunge wote kazi yao ni kuchukua hongo na hatakubali hiyo maneno, nikafurahi sana kama ameamua hivyo kwa sababu yeye mwenyewe ndiye mwenye kuhonga wabunge, nilifikiri hayo maneno ya hongo yamefika mwisho lakini sasa yameongezeka, pale ikulu ndio mahali kwa hongo na ufisadi”,alidai Gachagua
Wakati huo huo waziri wa usalama wa zamani Fred Matiang’i aliyeandamana na Gachagua aliomba wakenya kuwaunga mkono wanaoendeleza kamapeni za kumuondoa rais William Ruto mamlakani.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

