Connect with us

News

Gavana Sakaja taabani kuhusu hoja ya kubanduliwa mamlakani

Published

on

Zaidi ya Wawakilishi wadi 70 wa kaunti ya Nairobi walitia saini hoja ya kutokuwa na Imani na Gavana wa kaunti ya Nairobi Johnson Sakaja, ambayo inalenga kumbandua mamlakani iwapo hoja hiyo itapitishwa na bunge hilo.

Katika kikao cha siku ya Jumanne Agosti 25, 2025 katika bunge hilo ambacho kilihudhuriwa na Wawakilishi wadi 96 kati ya 122, Wawakilishi wadi hao walitia saini hoja hiyo ambayo pia inalenga kumtema nje Naibu Gavana wa kaunti hiyo James Muchiri.

Kikao hicho kilichoongozwa na Spika wa bunge hilo Ken Ng’ondi pamoja na kiongozi wa walio wengi katika bunge hilo Peter Imwatok, Niabu Kiranja wa wachache katika bunge hilo Mark Mugambi na Waithera Chenge, kimeweka wazi ajenda za kumtimua Gavana Sakaja na Muchiri.

Wawakilishi wadi hao walisema Gavana Sakaja pamoja na Naibu wake walishindwa kusimamia vyema raslimali za kaunti, ukiukaji wa Katiba, utumizi mbaya wa ofisi ya umma miongoni mwa masuala mengine ibuka.

Iwapo hoja hiyo itafaulu katika mchakato wa kumtimua Gavana Sakaja na naibu wake, basi moja kwa moja spika wa bunge hilo Ken Ng’ondi atachukua nafasi ya ugavana kwa kipindi cha siku 60 kabla ya uchaguzi wa ugavana kufanyika.

Hayo hayo yatategemea iwapo hoja hiyo itapitishwa katika bunge hilo baada ya Wawakilishi wadi wa Nairobi watakaporejelea vikao vya bunge mwezi Septemba na iwapo bunge la Seneti kwa kuzingatia kanuni za Katiba itaidhinisha hoja hiyo ya Wawakilishi wadi.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending