Connect with us

News

Gavana wa Isiolo Abdi Guyo atimuliwa Mamlakani

Published

on

Bunge la kaunti ya Isiolo limembandua Mamlakani Gavana wa kaunti hiyo Abdi Ibrahim Guyo.

Hii ni baada ya Wawakilishi wadi 16 kati ya 18 katika bunge la kaunti hiyo kupiga kura ya kutokuwa na Imani na Gavana Guyo na kumtimua mamlakani.

Kulingana na hoja iliyowasilishwa katika bunge hilo na Mwakilishi wadi wa Sericho Abubakar Godana tangu mwezi Juni tarehe 10 ilikashifu uongozi duni wa Gavana Guyo.

Shtuma zengine zilizochangia kubanduliwa Mamlakani kwa Gavana Guyo ni pamoja na utumizi mbaya wa ofisi ya umma, ufisadi, ukiukaji wa sheria, kukwama kwa miradi muhimu ya maendeleo, kushindwa kuafikia malengo ya mapato, uteuzi wa washauri 36 na maafisa wakuu 31  licha ya kaunti hiyo kupokea mgao wa tatu wa mapato nchini miongoni mwa masuala mengine.

Hata hivyo hoja ya kumbandua mamlakani Gavana Guyo iliendelea katika bunge la kaunti hiyo licha ya Mahakaka kuu ya Isiolo kuidhinisha kusitishwa kwa hoja hiyo hadi masuala tata yatatuliwe.

Hoja ya kubanduliwa Mamlakani kwa Gavana huyo sasa imewasilishwa katika bunge la seneti kwa kuzingatia kipengele cha 181 cha Katiba ya nchi na sehemu ya 33 ya sheria za serikali za kaunti.

Kutimuliwa kwa Gavana Guyo mamlakani kuongeza idadi ya magavana waliotemwa uongozini akiwemo aliyekuwa Gavana wa Nairobi Mike Mbuvi Sonko, aliyekuwa Gavana wa Kiambu Ferdinand Waititu, aliyekuwa Gavana wa Meru Kawira Mwangaza na sasa ni Gavana wa Isiolo Abdi Ibrahim Guyo.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending