News
Gavana wa Kericho Eric Mutai abanduliwa mamlakani
Gavana wa kaunti ya Kericho Eric Mutai amebanduliwa mamlakani kupitia hoja ya kutokuwa na Imani naye.
Jumla ya Wawakilishi wadi 33 kati ya 47 wa bunge la kaunti hiyo waliunga mkono hoja ya kumuondoa mamlakani.
Kikao hicho maalum kilizua mjadala mkali kabla ya kura kupigwa huku mivutano ya kisaisa ikishuhudiwa wakati wa kura hiyo na kupelekea Wawakilishi wadi wawili wa kaunti hiyo kujeruhiwa na kupelekea hospitalini.
Mutai anakabiliwa na shtuma za kutumizi mbaya wa mamlaka, kujinufaisha binafsi na miradi ya umma, ukiukaji wa Katiba na usimamizi mbaya wa rasilimali za kaunti hiyo.
Hatua hiyo imetokea siku ya mwisho ya kongamano la Ugatuzi la kutathminu ufanisi na changamoto za utawala hali ambayo inamuweka Gavana Mutai hatima yake kuwa mikononi mwa bunge la Seneti.

Vikao vya bunge la kaunti ya Kericho
Wakati wa kongamano hilo aliyekuwa Waziri mkuu Raila Odinga kwenye hotuba yake aligusia migogoro ya uongozi baina ya magavana na Wawakilishi wadi hali inayoathiri Serikali za Ugatuzi, malengo na mchango mkubwa uliokusudiwa kuimarisha maendeleo Mashinani.
Taarifa ya Eric Ponda
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

