Connect with us

News

Gharama ya matibabu na uhaba wa dawa umeathiri juhudi za kudhibiti ugonjwa wa figo

Published

on

Ulimwengu umeadhimisha siku ya kimatiafa ya Figo dunianihuku ikibainika kuwa gharama kubwa za matibabu pamoja na uhaba wa dawa katika hospitali za umma nchini ni miongoni mwa changamoto kuu zinazokwamisha juhudi za kukabiliana na ugonjwa wa figo.

Wagonjwa wa figo waliopata matibabu na wanaoendelea kutumia dawa walisema hali hiyo imefanya matibabu kuwa mzigo mkubwa kwao na familia zao.

Wakizungumza wakati wa maadhimisho ya siku ya Figo duniani yaliyofanyika katika uwanja wa Karisa Maitha mjini Kilifi, kaunti ya Kilifi, wagonjwa hao waliitaka serikali kuingilia kati ili kupunguza gharama za matibabu na kuhakikisha dawa zinapatikana kwa urahisi katika hospitali za umma.

Aidha, wagonjwa hao walilalamikia ukosefu wa taasisi za kupandikiza figo nchini wakisema hali hiyo inalazimu baadhi yao kusafiri hadi mataifa ya nje ili kupata huduma hiyo, jambo linaloongeza gharama na kuchelewesha matibabu.

Kwa upande wao, wauguzi wa ugonjwa wa figo wakiongozwa na Daniel Masha pamoja na Fatuma Bashir walikiri kuwepo kwa changamoto hizo huku wakisema kuna haja ya serikali kubuni mikakati madhubuti ya kuhakikisha gharama za matibabu ya figo zinadhibitiwa kikamilifu kupitia mpango wa Bima ya Afya ya Jamii (SHA).

Masha pia alipendekeza kuanzishwa kwa taasisi maalum za kupandikiza figo katika kila kaunti, pamoja na kuajiri wataalamu wa kutosha ili kuboresha huduma kwa wagonjwa wa figo nchini.

Naye mtaalamu wa afya ya figo, Daktari Andrew, alisisitiza umuhimu wa kuongeza hamasa kwa umma kuhusu ugonjwa wa figo. Amesema uhamasishaji utasaidia wananchi kutambua dalili mapema na kuchukua hatua za matibabu kwa wakati.

Daktari Andrew pia aliwahimiza wananchi kujenga utamaduni wa kufanyiwa uchunguzi wa afya mara kwa mara, akipendekeza kila mtu kutembelea kituo cha afya angalau mara moja kwa mwaka kwa ajili ya uchunguzi wa jumla wa afya.

Maadhimisho ya siku ya Figo duniani hufanyika kila mwaka kwa lengo la kuongeza uelewa kuhusu magonjwa ya figo, umuhimu wa kinga, na upatikanaji wa matibabu kwa wagonjwa duniani kote.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Ethekon: Uchaguzi mkuu utakuwa huru, haki na uwazi

Published

on

By

Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC imeanza rasmi zoezi la kuwasajili wapiga kura wapya kote nchini, huku ikilenga kuwasajili wapiga kura milioni 6.2, kabla ya uchaguzi mkuu ujao. 

Mwenyekiti wa Tume hiyo Erastus Ethekon aliwahakikishia wakenya kwamba makamishna wa tume hiyo watahakikisha uchuguzi mkuu ujao unakuwa huru, haki na uwazi.

Akizungumza katika kaunti ya Kwale wakati wa kuzindua wa zoezi la usajili wa wakipiga kura kote nchini, Ethekon alisema serikali imewekeza raslimali za kutosha za kufanikisha zoezi hilo.

“Nataka kuwahakikishia wakenya kwamba tumejipanga kama IEBC na tuko na raslimali za kutosha kuhakikisha zoezi la usajili wa wapiga kura linaendeshwa vyema na uchaguzi mkuu utakuwa huru, haki na wazi ili kuhakikisha wakenya wanatekeleza jukumu lao la kidemokrasia na hatua hiyo tutafikia idadi ya wapiga kura zaidi ya milioni 27”, alisema Ethekon.

Naye Naibu Mwenyekiti wa IEBC Fahima Araphat alisema tayari maafisa wapya wa IEBC elfu 12 wameajiriwa kuhakikisha zoezi hilo liendeshwa vyema ili kusajili idadi kubwa ya wapiga kura

“Sisi tunafanya kazi yetu bila kuegemea upande wowote wa kisiasa na tuko tayari kuhakikisha anashinda uchaguzi anatangazwa mshindi kwa haki, na kama tuko na makarani elfu 12 na wote wasajili wapiga kura wapya elfu 10 kila moja tutakuwa na idadi kubwa ya wapiga kura, sasa hiyo ndio tunalenga kupata”, alisema Fahima.

Kwa upande wake Gavana wa kaunti ya Kwale Fatuma Achani, aliipongeza tume hiyo kwa zoezi hilo endelevu la wapiga kura, akisema ni hatua ya kipekee kwa jamii ambazo zimekosa fursa ya kujisajili kama wapiga kura.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

IEBC yasema idadi ya wanaojisajili ni ndogo mno

Published

on

By

Zoezi endelevu la usajili wa wapiga kura kote nchini limeng’oa nanga huku maafisa wa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC wakilenga idadi kubwa ya vijana katika zoezi hilo.

Katika kaunti ya Kilifi eneo bunge la Kilifi Kazkazini, zoezi hilo limefanyika katika vituo vinne tofauti huku idadi ndogo ya wapiga kura ikishuhudiwa licha ya vuguvugu la TUKO KADI kuanzishwa na vijana ili kuwajisajili wapiga kura.

Akizungumza na Wanahabari wakati wa zoezi hilo, Naibu Afisa wa usajili wa wapiga kura katika eneo bunge la Kilifi Kazkazini Abdul Mohammed aliwarai vijana kujitokeza kwa wingi na kujisajili.

Mohammed pia aliwarai vijana kukoma kutumiwa vibaya na wanasiasa kwa manufaa yao binafsi, akipongeza vuguvugu lilionzishwa na vijana la TUKO KADI kama njia moja ya kuwahamasisha vijana kujisajili kama wapiga kura.

“Tumeanza zoezi hili na tunawahimiza vijana wajitokeze kwa wingi na kujisajili kama wapiga kura ili kutumia nafasi hiyo kuchagua viongozi wanawataka na wala wasikubali kutumiwa vibaya na wanasiasa”, alisema Mohammed.

Kwa upande wao baadhi ya vijana waliojisajili waliwarai vijana wenzao kujitokeza kwa wingi na kushiriki zoezi hilo ili kuchagua viongozi wanaohisi wataleta maendeleo sawa na kubuni nafasi za ajira.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading

Trending