News
Hospitali ya Rufaa ya kaunti ya Kilifi yafanikisha uzalishaji wa mapacha walioshikana
Hospitali ya Rufaa ya kaunti ya Kilifi imepata mafanikio ya kihistoria ya kitabibu baada ya kufanikisha uzalishaji watoto mapacha walioshikana kwa mara ya kwanza.
Watoto hao mapacha ambao walioshikana katika sehemu ya tumbo, wako katika hali salama pamoja na mama yao kwani shughuli hiyo ya uzalishaji ilifanywa kwa ustadi wa hali ya juu.
Wataalamu wa kiafya walifanikisha uzalishaji huo wa watoto mapacha walioshikana ni pamoja na Daktari Sumeiya wa magonjwa ya Wanawake, Daktari Kadivani wa upasuaji wa watoto, Daktari Kalama wa kuhudumia watoto pamoja na usaidizi wa wauguzi wa wodi za uzazi.
Daktari mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya kaunti ya Kilifi, Dkt. Gilbert Angore, waliwapongeza madaktari waliofanikisha shughuli hiyo, akisema Mama na watoto hao wako katika hali nzuri na watasafirishwa hadi Hospitali kuu ya kitaifa ya Kenyatta jijini Nairobi kwa uangalizi zaidi.

Madaktari wa Hospitali ya Rufaa ya kaunti ya Kilifi wakiongozwa na Daktari mkuu Gilbert Angore wakiwa na Jemimah Sidi Nzai ambaye ni mama wa mapacha walioshikana
Hata hivyo mama wa watoto hao Jemimah Sidi Nzai alielezea jinsi alivyopokea matibabu hadi ya kujifungua watoto hao mapacha walioshikana, akielezea matumani yake ya kupata matibabu zaidi katika hospitali kitaifa ya Kenyatta jijini Nairobi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

