News
IEBC imesajili wakenya 250,391 katika zoezi la usajili wa wapiga kura
Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC imesema kufikia sasa, imesajili wakenya 250, 391 na kufikia idada ya wakenya waliosajili kuwa 22,352,923.
Kamishna wa Tume hiyo Alutalala Mukhwana alisema idadi hiyo inajumuisha asilimia 50.9 ya wanaume na asilimia 49.1 ikiwa na wanawake huku asilimia 67.35 ikiwa na wale wa umri wa miaka 35 na zaidi huku asilimia 32 ikiwa wale wa chini ya miaka 35.
Alutalala alisema idadi hiyo inaonyesha wazi kwamba usajili wa vijana kama wapiga kura iko chini mno, akisisitiza haja ya vijana kujitokeza kwa wingi kupitia shinikizo la Niko Kadi na kusajili idadi kubwa ya wapiga kura.
Aidha alidokeza kwamba japo baadhi ya wakenya wametambua haki ya upigaji kura kupitia hamasa mbalimbali, wengi wanaojitokeza na wale wanaoishi katikati ya miji mikuu, akiwarai wananchi walio vijiji pia kujisajili.
Wakati huo huo alidokeza kwamba ili Tume ya IEBC iandea uchaguzi huru, haki na usawa ni lazima, maafisa na makamishna wa tume hiyo wapewe mazingira bora ya kujiandaa na wala sio wanasiasa na wananchi kuikosoa tume hiyo kila mara.
“Ili kufanikisha uchaguzi huru haki na usawa ni lazima tupewe mazingira safi, salama na yenye amani kwa sababu kuandaa uchaguzi sio jambo rahisi kwani linahitaji mikakati bora lakini hapa kwetu sio wanasiasa ama wananchi wako na fikra tofauti kabisa kwa sisi maafisa wa IEBC”, alisema Alutalala.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

