Connect with us

International News

Israel na Marekani zazidisha mashambulizi dhidi ya Iran

Published

on

Kwa siku ya tano mfululizo Jeshi la Israel kwa ushirikiano na Marekani, limefanya mashambulio mapya katika ardhi ya Iran dhidi ya kile imekitaja kuwa kuangamiza kabisa utawala wa kigaidi huku ikiionya Iran kujiandaa kwa mashambulio makubwa zaidi yatakayoisambaratisha miundombinu ya kijeshi ya nchi hiyo.

Mashambulio hayo ya usiku wa kuamkia leo Machi 4, yalilenga mji Tehran na Beirut, kama mwendelezo wa hujuma nzito za kijeshi baada ya lile shambulio la Februari 28, lililomuua kiongozi wa kidini Ayatola Ali Khameni.

Mwendelezo huo wa mashambilizi sasa yanaifikisha idadi ya watu waliouawa katika pande zote mbili takribani watu 700.

Mataifa kama vile Ufaransa, Urusi, na China yalitoa wito wa kusitishwa kwa haraka vita hivyo, lakini kauli ya Rais wa Marekani Donald Trump haionyeshi dalili za kukomeshwa kwa mashambulio hayo baada ya kudokeza katika taarifa yake, kwamba vita hivyo huenda vikachukua zaidi ya wiki 5.

Kwa upande wake, Iran inazidisha mashambulizi yake dhidi ya taasisi muhimu za Israel na Marekani katika eneo la Mashariki ya kati na shambulio la hivi punde kabisa likilenga ubalozi wa Marekani huko Dubai na bandari Ya Fujairah.

Pia mashambulio hayo yanaendelezwa nchin Israel, ambako Idadi ya vifo vya Waisreali inazidi kuongezeka, ingawa hakuna taarifa kuhusu idadi kamili.

Viongozi wa juu wa Israel wamepiga marufuku kutangaza au kupiga picha mashambulizi yanayoyafanya ndani ya Israel.

Mashambilizi haya sasa yamesambaa katika eneo la Ghuba huku Mataifa ya kigeni yakianzisha mkakati wa kuwahamisha raia wao ambao wamekwama kufuatia kufungwa kwa anga za mataifa hayo.

Iran pia imefunga Mlango wa Bahari ya Hormuz ambayo ni muhimu kwa kupitisha takriban mapipa milioni 20 ya mafuta kila siku.

Hatua hii tayari imeathiri biashara ya kimataifa.

Taarifa ya Eric Ponda

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

International News

Vita dhidi ya Al-Shabab vya shika kasi Somalia

Published

on

By

Operesheni kali ya kijeshi inayoendelea nchini Somalia ambapo zaidi ya wanamgambo 33 wa kundi la Alshabab wameuawa katika eneo la Shabelle nyanda za chini za Jubaland.

Ufanisi wa operasheni hii ya hivi punde ni muendelezo wa oparesheni iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Aprili 24 katika eneo hilo la Juba ambapo Wanamgambo 27 wa AlShabab waliuawa.

Hii ina maana kwamba Jeshi la Somali limefanikiwa kuvunja maficho muhimu ya kundi hilo, ambalo kufikia sasa ya Wanamgambo 60 wameuawa

Kwa mujibu wa vianzo vya habari hususan kutoka kwa maafisa wa usalama, operesheni hiyo inafanyika kufuatia taarifa za kijasusi kuhusu maficho ya wanamgambo hao waliokuwa wakipanga mashambulizi dhidi ya vituo muhimu na taasisi za serikali.

Wanajeshi hao walivamia ngome za magaidi hao kwa ustadi mkubwa, wakifanikiwa kudhibiti eneo hilo baada ya mapambano makali yaliyochukua muda wa saa kadhaa.

Maafisa wamesema kuwa mafanikio hayo ni sehemu ya juhudi zinazoendelea za kuimarisha usalama na kuangamiza kabisa mtandao wa Al-Shabaab ambao kwa muda mrefu umekuwa ukihatarisha amani katika maeneo mbalimbali ya Somalia na ukanda mzima wa Afrika Mashariki.

Wananchi wa eneo la Jubbaland wameelezea matumaini mapya kufuatia operesheni hiyo, wakisema kuwa hatua hiyo inaleta nuru ya kurejea kwa utulivu na maendeleo baada ya miaka ya hofu na mashambulizi ya mara kwa mara nchini.

Serikali imeapa kuendeleza msako dhidi ya wanamgambo hao hadi pale watakapokomesha kabisa vitisho vya mashambulio , huku ikiwataka wananchi kushirikiana na vyombo vya usalama kwa kutoa taarifa zitakazosaidia kudhibiti ugaidi.

Taarifa ya Billy Mongo

Continue Reading

International News

Kumbukumbu za muaji ya kimbari Rwanda

Published

on

By

Ni miaka 32 tangu kutokea kwa mauaji ya kimbari nchini Rwanda.

Leo, tarehe saba Aprili, raia wa Rwanda pamoja na dunia kwa ujumla wanaungana kukumbuka kuanza kwa mauaji ya kimbari ya mwaka 1994, ambapo zaidi ya watu laki nane, wengi wao wakiwa jamii ya Watutsi, waliuawa ndani ya kipindi cha siku mia moja.

Tarehe hii ni ya kihistoria kwa taifa hilo ambalo miaka 32 iliyopita lilikumbwa na moja ya matukio ya kikatili zaidi katika historia ya mwanadamu.

Mauaji hayo yalichochewa na kuuawa kwa aliyekuwa rais wa Rwanda Juvenal Habyarimana, tukio lililosababisha kuzuka kwa vurugu kote nchini.

Kilichofuatia ni mashambulizi ya kimbari kati ya Wahutu na Watutsi, ambapo zaidi ya watu milioni moja wanaripotiwa kupoteza maisha katika muda wa siku mia moja.

Wanawake, wanaume na watoto walilengwa katika mashambulizi hayo yaliyopangwa, jamii zikivunjika na dunia ikishuhudia tukio hilo kwa muda bila kuchukua hatua za haraka kuzuia maafa hayo.

Katika kuadhimisha siku hii, inayojulikana kama KWIBUKA, yenye maana ya “tunakumbuka,” bendera nchini Rwanda zinapepea nusu mlingoti, huku Rais Paul Kagame akitarajiwa kuwasha mwenge wa kumbukumbu katika makavazi ya Kigali.

Hata hivyo, licha ya historia hiyo ya maumivu, Rwanda imepiga hatua kubwa katika kipindi cha miongo mitatu iliyopita, ikijijenga upya kutoka jamii iliyogawanyika hadi kuwa taifa lenye umoja, likishuhudia maendeleo ya kijamii na kiuchumi pamoja na juhudi za maridhiano na haki kwa wahanga.

Leo hii, Rwanda inasimama kama mfano kwa mataifa mengine aduniani, huku wito wa kuhakikisha mauaji ya kimbari hayajirudii tena ukiendelea kusisitizwa.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

Trending