Connect with us

News

Jamii ya Wapokomo yalalamikia uongozi wa Mombasa

Published

on

Jamii ya wapokomo wanaoishi kaunti ya Mombasa wamelalamikia kutengwa na serikali ya kaunti hiyo kwa kile wanachodai kuwa ni ubaguzi wa kikabila.

Wakiongozwa na mwenyekiti wao, Abdhalla Bakar, walisema licha ya kuishi Mombasa kwa muda mrefu na kuwa wapiga kura katika kaunti hiyo, jamii hiyo haijawahi kuhusishwa ipasavyo katika mipango ya maendeleo, wala kuteuliwa kwenye nafasi muhimu za kiutawala.

Kwa mujibu wa Bakar, jamii ya Wapokomo imeendelea kusahaulika katika upangaji wa bajeti, utoaji wa zabuni, ajira, na huduma muhimu za kijamii.

“Serikali zote za Mombasa huwa hazitutambui, dhana ni kwamba sisi huenda kupiga kura kwetu lakini sisi zaidi ya kura elfu 20 huwa tunazipiga hapa Mombasa, lakini ukienda kwa serikali ya kaunti hatuna mfanyakazi yeyote kutoka kwa jamii ya Chanamaro, ukienda kwa wanasiasa hatuna hata diwani”, alisema Bakar.

Kwa upande wake mbunge wa eneo bunge la Galole kaunti ya Tana River Said Hiribae alieleza masikitiko yake kuhusu suala hilo, akiitaka serikali ya kaunti ya Mombasa kuhakikisha inajumuisha jamii zote bila ubaguzi.

“Hapa Mombasa kabila hizi kunazaidi ya kura elfu 20, na hizo kura elfu 20 zote hazijawasaidia Chanamaro, kwa sababu ukiangalia kabila zingine pengine wanaweza kupata wacha uwakilishi wadi, hata ubunge pia wangepata”, alisema Hiribae.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending