Connect with us

News

Jamii ya Wapokomo yalalamikia uongozi wa Mombasa

Published

on

Jamii ya wapokomo wanaoishi kaunti ya Mombasa wamelalamikia kutengwa na serikali ya kaunti hiyo kwa kile wanachodai kuwa ni ubaguzi wa kikabila.

Wakiongozwa na mwenyekiti wao, Abdhalla Bakar, walisema licha ya kuishi Mombasa kwa muda mrefu na kuwa wapiga kura katika kaunti hiyo, jamii hiyo haijawahi kuhusishwa ipasavyo katika mipango ya maendeleo, wala kuteuliwa kwenye nafasi muhimu za kiutawala.

Kwa mujibu wa Bakar, jamii ya Wapokomo imeendelea kusahaulika katika upangaji wa bajeti, utoaji wa zabuni, ajira, na huduma muhimu za kijamii.

“Serikali zote za Mombasa huwa hazitutambui, dhana ni kwamba sisi huenda kupiga kura kwetu lakini sisi zaidi ya kura elfu 20 huwa tunazipiga hapa Mombasa, lakini ukienda kwa serikali ya kaunti hatuna mfanyakazi yeyote kutoka kwa jamii ya Chanamaro, ukienda kwa wanasiasa hatuna hata diwani”, alisema Bakar.

Kwa upande wake mbunge wa eneo bunge la Galole kaunti ya Tana River Said Hiribae alieleza masikitiko yake kuhusu suala hilo, akiitaka serikali ya kaunti ya Mombasa kuhakikisha inajumuisha jamii zote bila ubaguzi.

“Hapa Mombasa kabila hizi kunazaidi ya kura elfu 20, na hizo kura elfu 20 zote hazijawasaidia Chanamaro, kwa sababu ukiangalia kabila zingine pengine wanaweza kupata wacha uwakilishi wadi, hata ubunge pia wangepata”, alisema Hiribae.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending