Connect with us

News

Kamati ya elimu katika bunge la kitaifa yamkosoa Bitok kwa kususia kikao chao

Published

on

Kamati ya elimu katika bunge la kitaifa limekashfu vikali hatua ya Katibu katika Wizara ya elimu nchini Julius Bitok, kushindwa kufika mbele ya Kamati hiyo kujadili mapendekezo ya bajeti ya mwaka wa fedha 2027/2028.

Akizungumza baada ya kuhairishwa kwa kikao hicho, Mwenyekiti wa kamati hiyo Julius Melly, alisema kwamba kutofika kwa Katibu huyo  ni dharau kwa kamati hiyo na kunaashiria mwenendo wa kutoheshimu wito wa kamati, akiongeza kwamba sio mara ya kwanza kwa afisa huyo kushindwa kufika au kutoa majibu ya kuridhisha kuhusu masuala nyeti yanayohusu sekta ya elimu.

Kamati hiyo ilisema kuwa ilitoa mwaliko rasmi kwa Makatibu wote husika kufuatia kuwasilishwa kwa taarifa ya sera ya bajeti bungeni tarehe 11 Februari, ikionyesha wazi tarehe, mahali na ajenda ya kikao hicho kwa kuzingatia matakwa ya Sheria ya Usimamizi wa Fedha za Umma.

Ingawa maafisa wengine waliomba udhuru kupitia njia rasmi na wakaruhusiwa, Bitok hakufika wala kutoa maelezo ya kuridhisha, hali iliyolazimu kamati kusubiri baada ya kukamilisha kikao cha awali na Tume ya kuwaajiri Walimu nchini TSC.

Sasa kamati hiyo ilitoa wito rasmi wa kumtaka afike mbele ya kamati hiyo ikionya kuwa endapo hatahudhuria hatua za kinidhamu zitachukuliwa dhidi yake.

Melly alisema kamati haitavumilia dharau kwa Bunge wala uzembe katika kushughulikia masuala yanayogusa sekta muhimu nchini haswa elimu.

Wabunge walisema kutofika kwa Bitok kumechelewesha majadiliano kuhusu changamoto muhimu zinazoikumba sekta ya elimu, zikiwemo msongamano wa wanafunzi shuleni, changamoto za mpito wa wanafunzi kwenye mtaala wa CBE, ukosefu wa bima kwa wanafunzi, ucheleweshaji wa fedha za ruzuku, na hali ya jumla ya usimamizi wa shule.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending