News
Kampuni ya Simba Cement yafungwa, Kaloleni
Serikali ya kaunti ya Kilifi kwa ushirikiano na Wizara ya Madini imesitisha rasmi shughuli zote za uchimbaji madini zinazotekelezwa na kampuni ya Simba Cement eneo la Kaloleni kaunti ya Kilifi.
Agizo hilo limetolewa na Gavana wa kaunti ya Kilifi Gideon Mung’aro pamoja na Waziri wa madini na raslimali za uchumi wa bahari nchini Ali Hassan Joho, wakisema kampuni hiyo imeshindwa kufuata sheria za mazingira na haiwafaidi wakaazi wa eneo hilo.
Viongozi hao walisema shughuli za uchimbaji wa kampuni hiyo zimekuwa zikiathiri mazingira na wakazi wa maeneo ya karibu, huku wakiahidi kwamba serikali haitavumilia ukosefu wa uwajibikaji unaotishia afya na maisha ya wananchi.
Walisisitiza kwamba kampuni hiyo haitaruhusiwa kuendelea na shughuli zake hadi pale itakapokidhi masharti yote ya kisheria na kuthibitisha kwamba haileti madhara kwa binadamu wala mazingira.
“Hii kampuni wacha nikuambie waziri haisadii wananchi wa Kilifi kwa chochote waziri, na leo hii watu wa kambe ribe mnisikize na mnisikize kwa makini, vile nilifanya Jaribuni ndivyo nitakavyofanya leo, kuanzia kesho asubuhi na nitawafuata na barua kesho mwelezeni mwajiri wenu kwamba hii kampuni tumeifunga na nitawafuata na barua”, alisema Gavana Mung’aro.
Hatua hii iliungwa mkono na baadhi ya viongozi wa jamii na wanaharakati wa mazingira, wakisema kuwa ni wakati wa kuwajibisha wawekezaji wanaokiuka haki za wananchi kwa msingi ya maendeleo.
Simba Cement, ambayo imekuwa ikihusishwa na miradi mikubwa ya ujenzi, sasa inalazimika kukabiliwa na masharti mapya kabla ya kurejelea shughuli zake za kawaida.
Taarifa ya Elizabeth Mwende
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

