News
Kanja aagizwa kuwasilisha stakabadhi za Polisi kwa NPSC
Huduma ya kitaifa ya polisi nchini NPS iliagizwa kukabidhi orodha ya malipo ya polisi na kazi zote zinazohusiana na raslimali za umma kwa Tume ya kitaifa ya huduma ya polisi nchini NPSC.
Agizo hilo lilitolewa na Kamati ya bunge la kitaifa kuhusu uhasibu wa umma inayoongozwa na Mbunge wa Butere Tindi Mwale ambayo ilimuagiza Inspekta Jenerali wa polisi Douglas Kanja kutekeleza agizo hilo mara.
Kulingana na kamati hiyo, hatua hiyo itapunguza uhasama uliopo kati ya taasisi hizo mbili za umma huku ikimtaka Kanja kuhakikisha pia anawasilisha orodha ya mishahara sawa na kuruhusu tume hiyo kutekeleza majuku yake kwa mujibu wa katiba.
Hata hivyo Inspekta Jenerali wa polisi nchini Douglas Kanja aliahidi kutekelezwa kwa maagizo hayo huku mkurugenzi mkuu wa Tume ya huduma ya kitaifa ya polisi nchini NPSC Peter Lelei akiahidi kuandikia Kamati hiyo barua kuhakikisha iwapo maagizo hayo yametekelezwa.
Kanja alikuwa aliitwa mbele ya kamati hiyo kufuatia ripoti iliyotolewa na Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali Magaret Nyakang’o iliyoashiri kwamba NPSC haijaweza kutekeleza majukumu yake kwa kunyimwa stakabadhi muhimu.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

