Connect with us

News

Katana: Visa vya mauaji ya wazee kwa tuhma za uchawi vimepungua

Published

on

Visa vya mauaji ya Wazee kwa tuhma za uchawi vimetajwa kupungua kwa asilimia kubwa.

Mwenyekiti wa kituo cha Kaya Godoma Emmanuel Katana amesema eneo la Mrima wa Ndege eneo bunge la Ganze kaunti ya Kilifi, limekuwa sehemu ya kuwahifadhi wazee kutokana na visa hivyo.

Katana amesema idadi hiyo imepungua kutokana na hamasa za mara kwa mara zinazoendelezwa katika jamii, pamoja na vijana kuelimishwa kuhusu umuhimu wa kuwaenzi wazee wao.

Alisema kuwa vijana pia wamejumuishwa kwenye hamasa hizo ili kuhamasisha vijana wenzao kuhusiana na athari ya kuwaua wazee kwa shutuma za uchawi, akisisitiza haja ya vijana kuwa mstari wa mbele kueleza wenzao kwani wazee wamekuwa kielezo chema kwa jamii.

“Tumefanya hamasa kwa jamii na hatua hiyo imetusaidia sana kudhibiti visa vya wazee wetu kupoteza maisha yao kutokana na shtuma za uchawi, na tutaendelea kuwaelimisha vijana”, alisema Katana.

Mwenyekiti huyo pia alisema jamii imemudu kumaliz unyanyapaa kwani idadi kubwa ya wazee wamerejea makwao licha ya wao kunusurika kifo hapo awali wakihusishwa na uchawi.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Aisha Jumwa akihama rasmi chama cha UDA

Published

on

By

Mgombea wa kiti cha ugavana wa kaunti ya Kilifi Aisha Jumwa amekihama rasmi chama cha UDA, akisema atatangaza baadaye mwelekeo atakaochukua wa kisiasa.

Jumwa alitoa tangazo hilo katika kikao na Wanahabari kilichofanyika katika makaazi yake, eneo la Kakuyuni huko Malindi kaunti ya Kilifi leo siku ya Alhamis.

Hatua ya Jumwa ilijiri baada ya kuwepo na tetesi kwamba alikuwa na mipango ya kuhama chama hicho kutokana na sintofahamu za kisiasa ndani ya chama cha UDA kuhusu msimamo wake wa kisiasa wa kuwania nafasi ya ugavana wa Kilifi.

Jumwa alilalamika kwamba alikuwa akinyanyaswa na baadhi ya viongozi hata kutimuliwa katika Ikulu ya rais licha ya kupambana katika kampeni za rais Ruto mwaka wa 2022, akionekana kumlaumu rais Ruto kwa kutomjali tena hata baada ya kusimama na yeye kisiasa.

Kiongozi huyo alikashfu vikali kutengwa katika mikutano ya UDA licha ya kuwa mwandani wa rais Ruto na pamoja na kufanyikisha miradi ya serikali mashinani, akisema tangu atangaze mchakato wa kuwania kiti cha ugavana wa Kilifi mwaka wa 2027, amekuwa akipitia masaibu mengi.

Hii sio mara ya kwanza kwa Jumwa kukihama Chama cha UDA na kurejea kwenye chama hicho, lakini hatua aliyoichukua sasa itabadili masimamo wa kisiasa kaunti ya Kilifi.

Itakumbukwa kwamba Jumwa amekuwa mwandani wa karibu wa rais William Ruto, lakini hatua aliyoichukua huenda ikabadili msimamo wa kisiasa kaunti ya Kilifi na Pwani kwa jumla. 

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Mahakama ya Kilifi yaagiza kuzuiliwa Washukiwa 7 wa mauaji

Published

on

By

Mahakama ya Kilifi imeagiza kuzuiliwa kwa siku 14 washukiwa 7 wanaotuhmiwa kuhusika katika kifo cha mwanamke mmoja aliyekuwa na umri wa miaka 65, ambaye aliuwawa kwa tuhma za uchawi katika eneo la Malomani eneo bunge la Ganze kaunti ya Kilifi.

Washukiwa hao Gilbert Karisa Changawa, Selvestar Changawa Kahindi, Elizabeth Jackson Ngala, Dhahabu Kithi Kombe, Dzendere Palu Kalama, Agness Changawa na Kadzo Ngombo Bienge watazuiliwa katika kituo cha Bamba wakati uchunguzi ukiendelea.

Kulingana na Afisa mpelelezi kutoka kitengo cha DCI ameeleza mahakama kwamba ilikuwa mnamo tarehe 27 mwezi huu ambapo walipokea tarifa kwamba dama changawa alikuwa amekatwa kichwa na kuuwawa na watu wasiojulikana usiku huo.

Afisa mpelelezi pia ameeleza kuwa washukiwa ambao ni wanafamilia,siku kabla ya tukio husika walikuwa wameandaa kikao cha kudumisha Amani baada ya kifo kilichokuwa kimetokea kwa kijana mmoja mtoto wa mmoja kati ya washukiwa aliyefariki kaunti ya Mombasa baada ya kupigwa kwa tuhma za wizi.

Kutokana na kifo cha kijana huyo wanafamilia hao walimtuhmu dama kwamba ndiye aliyekuwa amemroga kijana huyo na kusababisha kifo hicho cha gafla, ambapo usiku huo Dama aliuwawa nyumbani kwake.

Washukiwa watarudishwa mahakamani tarehe 13 mwezi Agosti mwaka huu baada ya uchunguzi kukamilika.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading

Trending