Connect with us

News

Baadhi ya Wananchi wanataka walipwe kujisajili kuwa wapiga kura

Published

on

Afisa wa usajili wa tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC eneo bunge la Kilifi Kaskazini kaunti ya Kilifi , John Mwawasi amesema wanapania kusajili wapiga kura wapya 13,316 katika zoezi hilo ambalo linakamilika leo Aprili 28 baada ya kuanza Machi 30.

Katika mazungumzo ya kipekee na Coco FM kwenye afisi za IEBC hapa mjini Kilifi, Mwawasi alisema kufikia Aprili 27 walikuwa wamefanikiwa kusajili wapiga kura wapya 12,999 na kwamba muda wa usajili hautaongezwa baada ya kukamilika leo.

“Itakuwa vyema kama wakenya watajitokeza kwa wingi kabla ya zoezi hili kukamilika kwani IEBC haitaongeza muda licha ya Viongozi na baadhi ya wananchi kupendekeza muda zaidi kuongezwa” alisema Mwawasi.

Mwawasi alisema vijana wengi walijitokeza katika zoezi hilo huku akitaja baadhi ya changamoto ambazo wamezipitia katika usajili wa wapiga kura wapya.

“Baadhi ya wananchi hasa vijana wanalalamikia ukosefu wa vitambulisho na wengine kutaka kulipwa ili kujisajili kuwa wapiga kura”Aliongeza Mwawasi

Mwawasi pia alisema usajili wa wapiga kura utaendelezwa katika afisi za IEBC na vituo vya Huduma Center.

Wakaazi wa Kilifi Kazkazini wakishiriki zoezi la usajili wa wapiga kura

Kwa upande wa wananchi ambao walifika katika afisi za IEBC Kilifi Kaskazini walieleza namna zoezi hilo lilikuwa huku wakitoa wito kwa wakenya wengine kujisajili kwa wingi kuwa wapiga kura ili washiriki uchaguzi mkuu ujao wa mwaka wa 2027.

Haya yanajiri huku Tume (IEBC) ikifanya kila juhudi kufikia azma yake ya kuwaandikisha wapiga kura wapya milioni 2.5 na kaunti za Nairobi na Kiambu zinaongoza kwa idadi ya juu ya wapiga kura wapya.

Kaunti za Lamu, Isiolo na Mandera zikiandikisha idadi ya chini ya waliojisajili.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending