News
Mzozo wa ujenzi wa barabara ya Jaribuni waibuka tena
Mzozo kuhusu ujenzi wa barabara eneo la Jaribuni katika kaunti ya Kilifi unanukia tena miezi kadhaa baada ya wakaazi eneo hilo kufanya maandamano kulalamikia hali mbaya ya barabara licha ya wawekezaji kufaidika na raslimali za eneo hilo.
Wakaazi eneo hilo, sasa wanapinga mwingilio wa viongozi wanaotaka kumuondoa Mwanakandarasi anayeendelea na ujenzi wa barabara kutoka Jaribuni hadi Tezo, badala yake ujenzi huo uanzie Tezo hadi Jaribuni.
Wakaazi wa eneo hilo wakiongozwa na Mwakilishi wadi ya Jaribuni Peter Shehe wanatishia kuzuia mkandarasi kuendelea na ujenzi wa barabara hiyo, iwapo atahamishwa.
Kulingana na Mwakilishi wadi huyo eneo la Jaribuni kwa mda mrefu limekuwa likitoa bidhaa muhimu za ujenzi na shehemu ya barabara iliyosalia inafaa kukamilishwa kuanzia eneo hilo vyenginevyo wataandamana na kufunga timbo za wanakandarasi.

Mwakilishi wadi ya Jaribuni Peter Shehe akizungumza na Wanahabari kuhusu kuhamishwa kwa mwanakandari wa ujenzi wa barabara ya Jaribuni hadi Tezo
Wakaazi waliokongamana na Mwakilishi wadi eneo hilo wanadai waligundua Tinga Tinga za kutengeneza barabara zilikuwa zimeshitisha Shughuli zake, hali iliyowalazimu kuingilia kati wakimlaumu mbunge wa eneo hilo la Ganze Kenneth Tungule na mbunge wa Kilifi Kaskazini Owen Baya.

Wakaazi watishia kumzuia mwanakandarasi kuondolewa eneo hilo iwapo viongozi watasimamisha ujenzi wa barabara ya Jaribuni hadi Tezo
Wakaazi hao wanasema kwa mda mrefu wamelalamikia hali mbaya ya barabara licha ya eneo hilo kuwa na raslimali nyingi, wakisema kwa sasa hawatalaza damu na kuwacha mtui yeyote kuingia miradi ya eneo la Jaribuni.
Awali wakaazi wa Jaribuni waliandamana na kufunga barabara, hali iliyolazimu waziri wa Madini Ali Hassan Joho na Gavana wa Kilifi Gedion Mung’aro kuingilia kati, na kufanyikisha ujenzi wa barabara ya lami ya umbali wa Kilomita nane.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

