News
Mahakama yamuachilia mshukiwa wa unyakuzi wa ardhi
Mahakama ya Kilifi imemuachilia kwa dhamana ya shilingi laki tano na mdhamini wa kiasi sawa na hicho George Mweni Muramba anayekabiliwa na shtaka la unyakuzi wsa ardhi.
Mweni anadai kufanya usajili wa shamba mali ya Gulmohamed Khamis Shapi.
Hakimu wa Mahakama hiyo Ivy Wasike ametoa agizo hilo baada ya mshukiwa kukana madai yaliowasilishwa Mahakamani kwamba tarehe 21 mwezi Februri mwaka 2024 katika ofisi za usajili wa ardhi Kilifi kazkazini kaunti ya Kilifi, Mweni alifanya usajili wa ardhi nambari Kilifi/ Madeteni/367 akijua kuwa ardhi hiyo ilikuwa imeuziwa Gulmohamed Khamis Shapi.
Mahakama pia imeelezwa kwamba tarehe tofauti kati ya mwaka 2019 hadi 2022, Mweni alifanya ulaghai wa pesa shilingi milioni moja nukta nne [1,460,000] mali Andrew Kithi Kombe akisema kuwa angemuuzia ekari nusu ya ardhi hiyo ambayo haikuwa yake.
Vile vile mnamo tarehe tofauti ya mwezi Machi mwaka 2024, Mweni alimlaghai Judithi Adawo Otieno shilingi milioni nne nukta nne [4,400,000] akisema kuwa angemuuzia ekari 2.2 sehemu ya ardhi hiyo.
Kesi hiyo itasikizwa tarehe 23 mwezi Septemba mwaka huu wa 2026.
Taarifa ya Teclar Yeri
News
Aisha Jumwa akihama rasmi chama cha UDA
Mgombea wa kiti cha ugavana wa kaunti ya Kilifi Aisha Jumwa amekihama rasmi chama cha UDA, akisema atatangaza baadaye mwelekeo atakaochukua wa kisiasa.
Jumwa alitoa tangazo hilo katika kikao na Wanahabari kilichofanyika katika makaazi yake, eneo la Kakuyuni huko Malindi kaunti ya Kilifi leo siku ya Alhamis.
Hatua ya Jumwa ilijiri baada ya kuwepo na tetesi kwamba alikuwa na mipango ya kuhama chama hicho kutokana na sintofahamu za kisiasa ndani ya chama cha UDA kuhusu msimamo wake wa kisiasa wa kuwania nafasi ya ugavana wa Kilifi.
Jumwa alilalamika kwamba alikuwa akinyanyaswa na baadhi ya viongozi hata kutimuliwa katika Ikulu ya rais licha ya kupambana katika kampeni za rais Ruto mwaka wa 2022, akionekana kumlaumu rais Ruto kwa kutomjali tena hata baada ya kusimama na yeye kisiasa.
Kiongozi huyo alikashfu vikali kutengwa katika mikutano ya UDA licha ya kuwa mwandani wa rais Ruto na pamoja na kufanyikisha miradi ya serikali mashinani, akisema tangu atangaze mchakato wa kuwania kiti cha ugavana wa Kilifi mwaka wa 2027, amekuwa akipitia masaibu mengi.
Hii sio mara ya kwanza kwa Jumwa kukihama Chama cha UDA na kurejea kwenye chama hicho, lakini hatua aliyoichukua sasa itabadili masimamo wa kisiasa kaunti ya Kilifi.
Itakumbukwa kwamba Jumwa amekuwa mwandani wa karibu wa rais William Ruto, lakini hatua aliyoichukua huenda ikabadili msimamo wa kisiasa kaunti ya Kilifi na Pwani kwa jumla.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Mahakama ya Kilifi yaagiza kuzuiliwa Washukiwa 7 wa mauaji
Mahakama ya Kilifi imeagiza kuzuiliwa kwa siku 14 washukiwa 7 wanaotuhmiwa kuhusika katika kifo cha mwanamke mmoja aliyekuwa na umri wa miaka 65, ambaye aliuwawa kwa tuhma za uchawi katika eneo la Malomani eneo bunge la Ganze kaunti ya Kilifi.
Washukiwa hao Gilbert Karisa Changawa, Selvestar Changawa Kahindi, Elizabeth Jackson Ngala, Dhahabu Kithi Kombe, Dzendere Palu Kalama, Agness Changawa na Kadzo Ngombo Bienge watazuiliwa katika kituo cha Bamba wakati uchunguzi ukiendelea.
Kulingana na Afisa mpelelezi kutoka kitengo cha DCI ameeleza mahakama kwamba ilikuwa mnamo tarehe 27 mwezi huu ambapo walipokea tarifa kwamba dama changawa alikuwa amekatwa kichwa na kuuwawa na watu wasiojulikana usiku huo.
Afisa mpelelezi pia ameeleza kuwa washukiwa ambao ni wanafamilia,siku kabla ya tukio husika walikuwa wameandaa kikao cha kudumisha Amani baada ya kifo kilichokuwa kimetokea kwa kijana mmoja mtoto wa mmoja kati ya washukiwa aliyefariki kaunti ya Mombasa baada ya kupigwa kwa tuhma za wizi.
Kutokana na kifo cha kijana huyo wanafamilia hao walimtuhmu dama kwamba ndiye aliyekuwa amemroga kijana huyo na kusababisha kifo hicho cha gafla, ambapo usiku huo Dama aliuwawa nyumbani kwake.
Washukiwa watarudishwa mahakamani tarehe 13 mwezi Agosti mwaka huu baada ya uchunguzi kukamilika.
Taarifa ya Teclar Yeri

