Connect with us

News

Wahisani wajitokeza kumsaidia Magastone kuwa na makaazi mpya

Published

on

Katika kijiji cha Roka kumekuwa na pilkapilka za ujenzi wa nyumba ya kisasa ambao umetokea kivutio cha wengi kwani unafuatiliwa sana katika mitandao ya kijamii.

Shughuli za ujenzi wa nyumba ya makazi ya Magastone Baraka zilianza majuma kadhaa yaliyopita na wahisani ambao wamejitolea kumjengea Baraka nyumba nzuri ya kuishi.

Baraka alipata ajali mwaka wa 2020 alipoteleza na kuanguka bafuni alipokuwa akioga, ajali ambayo ilisababisha kuvunjika kwa mkono wake mmoja na baada ya miaka mitatu mkono wake huo ukalazimika kukatwa na kubadilikiwa na hali ya kuwakimu wazazi wake pamoja na mchumba wake.

Mambo yalipomzidia na kukumbwa na hali ngumu ya maisha aliziweka habari zake mitandaoni akiwaomba wahisani kumsaidia.

Wahisani mbalimbali waliitikia wito na kujitokeza kumsaidia akiwemo mgombea wa useneta Kilifi Wakili George Kithi, Presenter Kai na mkewe Diana Yegon, ambao wamefanikisha ujenzi wa nyumba hiyo ili kumuwezesha kufanikisha malengo yake ya kuwa na makaazi mapya.

Ujenzi wa Nyumba ya Magastone Baraka eneo la Roka Chumani kaunti ya Kilifi unaendelea

Wengine waliojitokeza kumsaidia na mafundi waliojitolea kuhakikisha Baraka anakuwa na nyumba huku mchango wa shilingi laki moja kutoka kwa Katibu katika Idara ya vijana na uchumi bunifu Fikirini Jacobs.

Mafundi pamoja na vibarua wanaendelea kukamilisha ujenzi wa nyumba ya vyumba viwili, sebule na jiko huku wasanii zaidi wakiahidi kumnunulia samani.

Huu ni mfano mzuri wa kutekelezwa kwa msemo wa Kiswahili nizike ningali Hai, usisubiri kuja kuweka mauwa kaburini.

Taarifa ya Lolani Kalu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wadau wa sekta ya uchukuzi wasitisha mgomo wao

Published

on

By

Maafisa wa sekta ya uchukuzi wameahirisha mgomo wao baada ya mazungumzo yaliyoongozwa na Rais William Ruto katika ikulu ya Mombasa.

Maafisa hao wakiongozwa na rais wa Muungano wa wamiliki wa matatu Albert Karagacha wamesema kuwa mengi ya masuala waliokuwa nayo ikiwemo kupanda kwa bei ya mafuta nchini yameangaziwa kwa kina na rais Ruto.

Karagacha amewataka wahudumu wa sekta ya uchukuzi wa umma pamoja na wamiliki wa magari ya uchukuzi wa mizigo kuhakikisha wanarudisha magari yao barabarani, akisema masuala waliowasilisha kwa rais yameangaziwa

Akizungumza mda mfupi baada ya kufanya kikao na rais William Ruto mjini Mombasa, Karagacha amesema serikali imekuwa kiangazia kwa kina masuala mbali mbali yanayohusu sekta ya uchukuzi nchini.

Aidha amesema iwapo bado serikali itakuwa inajikokota katika kufanikisha masuala waliojadiliana basi wataitisha mazungumzo zaidi na Wizara husika ili kuafikiwa kwa ajenda zao huku akisema japo suala la mzozo wa mafuta sio jambo la Kenya pekee lakini taifa inawajibu wa kusaidia wananchi wake.

Wakati huo huo Karagacha amewataka wakenya kutoingiza siasa katika suala la kupanda kwa bei ya mafuta nchini.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Mshukiwa wa ulanguzi na usafirishaji wa watoto anyimwa dhamana

Published

on

By

Mahakama ya Shanzu imemnyima dhamana mshukiwa wa ulanguzi wa watoto zaidi ya 20.

Mahakama imeagiza mshukiwa huyo kuzuiliwa rumande ili kuwawezesha maafisa wa polisi kukamilisha uchunguzi wao.

Mahakama imeelezwa kwamba mshukiwa huyo Almasi Rama Amos mwenye umri wa miaka 27 alikamatwa na maafisa wa upelelezi kutoka kitengo cha kupambana na ulanguzi wa binadamu na ulinzi wa watoto (AHTCPU) pamoja na maafisa wa idara ya upelelezi wa Jinai kutoka kaunti ya Mombasa.

Kukamatwa kwake kufuatia wiki kadhaa za uchunguzi kuhusu ripoti za unyanyasaji wa watoto zinazowalenga wasichana wadogo walio katika mazingira magumu.

Rama, anayetuhumiwa kwa kujihusisha na kundi linalodaiwa kuwa la ulanguzi wa watoto na dhulma za kingono na kufikishwa katika Mahakama ya Shanzu kufuatia operesheni ya kiusalama iliyoidhinishwa na maafisa hao.

Rama alipatikana katika mtaa wa Nguu Tatu eneo la Concordia katika kaunti ndogo ya Kisauni akiwa na watoto watatu wa kike.

Mahakama imeelezwa kuwa mshukiwa anadaiwa kuendesha “vituo vya uokoaji” katika kaunti za Mombasa na Kilifi kwa kujifanya kuwalea na kuwapa ushauri.

Kulingana na uchunguzi vituo hivyo vilikuwa vikitumika kama msingi wa dhulma za kingono na unyanyasaji wa watoto.

Alipokamatwa, mshukiwa aliwaongoza maafisa hadi kituo chengeni eneo la Ribe katika eneo bunge la Rabai, ambapo maafisa wa upelelezi waliwaokoa watoto 19 wa jinsia ya kike na kufikisha jumla ya waathiriwa waliookolewa kufikia ishirini na wawili (22).

Mbele ya Mahakama ya Shanzu tarehe 21 Mei, 2026, mshukiwa amekabiliwa na mfululizo wa mashtaka, ikiwemo unajisi, biashara ya watoto kwa madhumuni ya kuwadhulumu kingono pamoja na unyanyasaji wa watoto ambapo amekana mashtaka hayo.

 Kesi hiyo imepangwa kutajwa Juni 8, 2026.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading

Trending