News
Wahisani wajitokeza kumsaidia Magastone kuwa na makaazi mpya
Katika kijiji cha Roka kumekuwa na pilkapilka za ujenzi wa nyumba ya kisasa ambao umetokea kivutio cha wengi kwani unafuatiliwa sana katika mitandao ya kijamii.
Shughuli za ujenzi wa nyumba ya makazi ya Magastone Baraka zilianza majuma kadhaa yaliyopita na wahisani ambao wamejitolea kumjengea Baraka nyumba nzuri ya kuishi.
Baraka alipata ajali mwaka wa 2020 alipoteleza na kuanguka bafuni alipokuwa akioga, ajali ambayo ilisababisha kuvunjika kwa mkono wake mmoja na baada ya miaka mitatu mkono wake huo ukalazimika kukatwa na kubadilikiwa na hali ya kuwakimu wazazi wake pamoja na mchumba wake.
Mambo yalipomzidia na kukumbwa na hali ngumu ya maisha aliziweka habari zake mitandaoni akiwaomba wahisani kumsaidia.
Wahisani mbalimbali waliitikia wito na kujitokeza kumsaidia akiwemo mgombea wa useneta Kilifi Wakili George Kithi, Presenter Kai na mkewe Diana Yegon, ambao wamefanikisha ujenzi wa nyumba hiyo ili kumuwezesha kufanikisha malengo yake ya kuwa na makaazi mapya.

Ujenzi wa Nyumba ya Magastone Baraka eneo la Roka Chumani kaunti ya Kilifi unaendelea
Wengine waliojitokeza kumsaidia na mafundi waliojitolea kuhakikisha Baraka anakuwa na nyumba huku mchango wa shilingi laki moja kutoka kwa Katibu katika Idara ya vijana na uchumi bunifu Fikirini Jacobs.
Mafundi pamoja na vibarua wanaendelea kukamilisha ujenzi wa nyumba ya vyumba viwili, sebule na jiko huku wasanii zaidi wakiahidi kumnunulia samani.
Huu ni mfano mzuri wa kutekelezwa kwa msemo wa Kiswahili nizike ningali Hai, usisubiri kuja kuweka mauwa kaburini.
Taarifa ya Lolani Kalu
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

