Connect with us

News

Kaunti ya Kilifi yajitenga na shutma za Aisha Jumwa

Published

on

Serikali ya kaunti ya Kilifi imejitenga na vurugu zilizoshuhudiwa wakati wa mazishi ya Afisa wa kaunti katika eneo la Msabaha wadi ya Ganda eneo bunge la Malindi siku ya Jumatatu.

Akizungumza na vyombo vya habari, Naibu gavana wa Kilifi Flora Mbetsa Chibule, alidai kwamba wanasiasa wenye malengo fiche walitumia hafla ya mazishi na kutangaza semi za uongo kuhusu msaada wa kaunti kwa familia ya mwendazake.

Chibule alitangulia kwa kuomba msamaha kwa familia ya marehemu na kukariri kuwa serikali ya kaunti kupitia gavana Gedion Mung’aro awali iliwasiliana na familia kuhusu namna ya kuipa msaada, japo haukuwekwa hadharani.

Wakati huo huo Chibule alidokeza kwamba gavana Mung’aro binasfi alitoa msaada wake wa fedha kwa familia ya marehemu.

“Huyu ni mfanyakazi wa serikali ya kaunti mbali na mstahiki gavana wetu, idara ya ugatuzi na utekelezaji ilichangia kwa mambo hayo ya mazishi, alipokuwa na anaenda kuangaliwa maisha yake kule Moshi mustahiki gavana mwenyewe alitoa nusu milioni kumsaidi Baloteli(marehemu), nilikwenda pale tukaramuka(kuomboleza) tukasema mama madamu unahii shahada tutakutafutia nafasi katika serikali ya kaunti”, alisema Chibule. 

Vile vile naibu gavana huyo aliwapa changamoto viongozi wa siasa kuheshimu hafla za mazishi na kupunguza siasa hasa wanapoalikwa katika hafla hizo.

“Jana Msabaha mfanyakazi wetu shupavu almaarufu Baloteli nikwamasikitiko makuu ya kwamba matokeo ya mazishi yale yalikwenda vile yalivyo sisi kama serikali ya kaunti tunaomba msamaha kwa familia, kwa mama Mbeyu tusamehe kwa jinsi shughuli ilivyokuwa, viongozi wenzangu tafadhali mazishi yaheshimiwe”, alisistiza naibu gavana Chibule.

Katika hafla hiyo, Mwenyekiti wa bodi ya kitaifa ya barabara Aisha Jumwa alitoa changamoto kwa viongozi wa kaunti ya Kilifi kumpa ajira mke wa Marehemu kauli ambayo iliibua hisia miongoni mwa viongozi na kusababisha rabsha.

“Nimesikiza viongozi wa kaunti hapa mmoja mpaka wa mwisho wakizungumza, sikupata hata mmoja mwenye huruma aseme Baloteli ametumikia kaunti na hivi amefariki mkewe Maurine jumatatu au jumanne ako kazini, sikusikia, lakini mimi nilikuwa nimevipanga, mmkuja matangani na kama mmempangia simzunguze kila mtu asikie, lakini kwa sababu havikuzungumiziwa nimevipatia wiki moja kama hatapata kazi nitarejea hapa maana mwanijua mimi ni mtu wa matendo”, alisema Jumwa.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Rais Ruto atia saini kuwa sheria mswada wa hazina ya uwekezaji wa mali

Published

on

By

Rais William Ruto ametia saini kuwa sheria mswada wa hazina ya kitaifa ya uwekezaji wa mali (Sovereign Wealth Fund), hatua inayotajwa kuwa muhimu katika juhudi za Kenya za kuimarisha usimamizi wa fedha za umma, kulinda utajiri wa taifa na kuchochea ukuaji wa uchumi wa muda mrefu.

Utiaji huo wa saini ulifanyika katika Ikulu ya Nairobi na unaweka msingi wa kisheria wa kuanzishwa na kusimamiwa kwa mfuko wa taifa wa uwekezaji wa mali na kwamba unatarajiwa kuiwezesha nchi kuhifadhi rasilimali za umma zinazobaki baada ya matumizi ya kawaida, kufadhili uwekezaji wa kimkakati na kuimarisha uwezo wa uchumi kukabiliana na misukosuko ya kifedha siku zijazo.

Sheria hiyo mpya inaleta mfumo rasmi wa usimamizi wa utajiri wa taifa kwa kutenga akiba kwa ajili ya vizazi vijavyo, kuimarisha uthabiti wa uchumi na kufadhili uwekezaji katika miundombinu ya kimkakati ili kuongeza uimara wa kifedha nchini pamoja na kuhimiza matumizi yenye uwajibikaji ya rasilimali za umma.

Mfuko huo utatumika kuwekeza mapato ya ziada yanayotokana na rasilimali za asili na mali nyingine za umma, kwa lengo la kuhakikisha manufaa yake yanawanufaisha wananchi wa sasa na vizazi vijavyo.

Aidha, mfuko huo unakusudia kupunguza athari za changamoto za kiuchumi kwa kutoa kinga ya kifedha wakati wa misukosuko ya uchumi.

Sheria hiyo ni sehemu ya ajenda pana ya serikali ya mageuzi ya uchumi inayolenga kuimarisha usimamizi wa fedha za umma, kuongeza uwazi na kuendeleza maendeleo endelevu.

Pia, sheria hiyo imeweka mfumo wa uongozi na usimamizi wa mfuko huo, ukiwemo utaratibu wa kuhakikisha uwajibikaji, uwazi na usimamizi madhubuti katika uwekezaji na matumizi ya rasilimali za umma.

Maafisa wa serikali wameeleza kuwa Mfuko wa Taifa wa Uwekezaji wa Mali utakuwa na mchango mkubwa katika kufadhili miradi ya maendeleo yenye kipaumbele nchini huku ukihifadhi utajiri wa taifa kwa manufaa ya vizazi vijavyo.

Kupitishwa kwa sheria hiyo kunaiweka Kenya miongoni mwa mataifa yanayoongezeka duniani ambayo yameanzisha mifuko ya taifa ya uwekezaji wa mali kwa lengo la kulinda mali za taifa, kuimarisha uthabiti wa uchumi na kufadhili malengo ya maendeleo ya muda mrefu.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

IEBC yakosolewa dhidi ya masharti mapya kwa wanasiasa

Published

on

By

Kiongozi wa vijana katika Chama cha Wiper kaunti ya Kwale Nyawa Masai ameikosoa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC kutokana na masharti mapya iliyotoa dhidi ya wanasaisa kabla ya uchaguzi mkuu ujao.

Nyawa ameitaka Tume hiyo kuzingatia kanuni zake na taratibu za kuandaa uchaguzi na wala sio kila uchao kutoa masharti ambayo yanakinzana na majukumu ya Tume, akisema kuna taasisi zengine za umma zinafaa kuwajibika.

Akizungumza katika mkutano wa kisiasa katika eneo la Mwereni gatuzi dogo la Lungalunga kaunti ya Kwale, Nyawa aliesisitiza haja ya wanasiasa kupewa nafasi ya kuzungumza na wananchi sawa na kueleza sera zao bila ya vizuizi.

Kiongozi huyo wa vijana ambaye alitangaza nia yake ya kuwania kiti cha uwakilishi wadi ya Mwereni wakati wa uchaguzi ujao, amesema taifa la Kenya linazingatia demokrasia na kwamba kila taasisi inafaa kutekeleza majukumu yake.

“Katika uwaja wa siasa IEBC inakuzi moja tu kama msimamizi na kama msimamizi anaanza kutengeza sheria hapo ndipo anakosea, hii Kneya ni nchi ya demokrasia kwa hivyo IEBC isilete sheria nyingi na kufuatilia wanasiasa kuhusu pesa watatumia kwa kampeni, hiyo sio jukumu lake kuna taasisi inaitwa EACC”, alisema Nyawa.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending