Connect with us

News

Kaunti ya Kilifi yalemewa na madeni ya kima cha 12B

Published

on

Serikali ya kaunti ya Kilifi imebuni jopo la kuchunguza malimbikizi ya madeni ambayo yamedumu kwa muda mrefu bila ya wanakandarasi kulipwa zabuni zao.

Jopo hili lililoteuliwa na gavana wa kaunti ya Kilifi Gideon Maitha Mung’aro, linajukumu la kutathmini uhalali wa zabuni hizo huku kukiwa na shaka kuwa huenda baadhi ya kandarasi hizo zimetolewa kwa njia ya ulaghai.

Kaunti ya Kilifi ni miongoni mwa kaunti ambazo zinashtumiwa kwa malimbikizi ya madeni kwa wanakandarasi.

Bado kuna maswali mengi yanayokosa majibu kuhusiana na ongezeko la malimbikizi haya ya madeni ya kaunti ya Kilifi na utaratibu unaotumika kuwalipa wanakandarasi ambao sasa wanahoji ni vipi ulaghai huu ulivyotekelezwa pasi ya kuzingatiwa kwa utaratibu na mifumo ya kisheria katika utoaji wa zabuni.

Serikali ya kaunti ya Kilifi sasa inadaiwa takriban shilingi billioni 12 kwa mujibu wa ripoti ya hivi punde ya mkaguzi wa hesabu za serikali Nancy Gathungu.

Deni hilo linatokana na huduma za wanakandarasi ambao wametoa huduma kwa kaunti na baadhi yao wamekuwa wakidai pesa zao kwa zaidi ya miaka mitatu bila ya malipo.

Hali hii imetajwa kuchangia pakubwa kuzorota kwa uchumi wa kaunti ya Kilifi hasa ikizingatiwa mchango wa wafanyibiashara hao kwa uchumi wa kaunti.

Mbali na athari kubwa kwa uchumi na wanakandarasi wenyewe ni dhahiri kwamba miradi mingi ya maendeleo pia imekwama kutokana na makisio ya bajeti yasiyoendana na hali halisi ya mfuko wa bajeti wa kaunti.

Hivi majuzi Gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Maitha Mung’aro alifutilia mbali baadhi ya kandarasi na miradi ya maendeleo ili iweze kutathminiwa upya.

Uzinduzi wa ujenzi wa barabara za mashinani ulipewa wanakandarasi

Malimbikizi ya madeni haya ya mabilioni ya pesa pia yanatajwa kuchangia pakubwa msongo wa mawazo kwa baadhi ya wanakandarasi ambao wamejikuta wakiuziwa vyombo na mali zao ili kulipa mikopo waliotumia kufadhili kandarasi zao.

Hata hivyo wiki mbili zilizopita, kaunti ya Kilifi ilibuni Jopo maalum ya kuchunguza na kutathmini madeni hayo kabla ya kuidhinishwa kwa malipo.

Hali hii imeathiri kaunti nyingi ikiwemo kaunti ya Machakos ambako wanakandarasi wamelazimika kuandamana barabarani wakidai haki yao baada ya kusubiri malipo kwa muda nrefu.

Maandamano hayo yalipelekea maafisa wa usalama kutumia vitoa machozi kuwatawanya wanakandarasi hao huku baadhi yao wakikamatwa na kuwekwa korokoroni.

Taarifa ya Eric Ponda

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending