News
Kaunti ya Kilifi yasambaza tani 62.5 za Unga wa uji kwa shule za ECDE
Serikali ya kaunti ya Kilifi yaendeleza mpango wa kusambaza tani 62.5 za unga wa uji ulioimarishwa kwa virutubisho kwa vituo 813 vya umma vya ECDE, hatua itakayowanufaisha zaidi ya wanafunzi wa chekechea 50,000 katika kaunti nzima ya Kilifi.
Gavana wa kaunti ya Kilifi Gideon Maitha Mung’aro alisema mpango huo wa chakula pekee ni kati ya juhudi za kuhakikisha kila mtoto anapata lishe hasa akiwa shuleni.
Mung’aro amebainisha kupitia mtandao wake wa Facebook kwamba magari ya mizigo tayari yameelekezwa katika kaunti ndogo zote saba, yakigusa wadi zote 35 ili kuhakikisha kila kituo cha ECDE kinapokea mgao wake bila kuchelewa.
Katika Kituo cha chekechea kilichopo Fumbini, Wadi ya Kibarani, kaunti hii ya Kilifi gavana Mung’aro amesema maafisa wa kaunti walikagua shehena hiyo kama sehemu ya uzinduzi wa usambazaji. Ukaguzi huu uliashiria dhamira ya serikali ya kaunti katika uwajibikaji, uwazi na ustawi wa wanafunzi.
Maafisa kutoka Idara ya Elimu na idara ya Teknolojia na Mawasiliano ICT walibainisha kuwa mpango huu wa unga wa uji wenye virutubisho umebuniwa ili kuboresha lishe, mahudhurio shuleni, na umakini wa wanafunzi wa ECDE.
Serikali ya Kaunti ya Kilifi, kupitia Idara ya Elimu na ICT, itaendelea kuimarisha mpango wa chakula cha ECDE kama sehemu ya juhudi zake za kuendeleza elimu bora na ustawi wa mtoto katika kaunti ya Kilifi.
Taarifa ya Elizabeth Mwende
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

