News
Kaunti za Tanariver na Garissa zaathiriwa zaidi na mabadiliko ya tabia nchi
Muungano wa mashirika ya kukabilina na athari za mabadiliko ya tabia nchi chini ya mpango wa WISER KENYA umetaja kaunti za Tanariver na Garissa kama zinazoathirika mara kwa mara na mabadiliko ya tabia nchi.
Mkurugenzi wa mpango huo Phillip Omondi ambaye pia ni mwanasayasi wa masuala ya hali ya hewa, alidokeza kuwa kaunti hizo zimekuwa zikikumbwa na hali ya mafuriko na ukame kwa mda.
Akizungumza na Coco Fm, Omondi alisema kwa sasa wanaendelea na mikakati ya kuhamasisha jamii za sehemu hizo kuhusu namna ya kukabiliana na madhara hayo.
“Kaunti za Tanariver na Garissa ambako tunatekeleza mradi wa Wiser Kenya ni kaunti ambazo ziko katika hatari ya mafuriko na ukame, kwa hio serikali ya Uingereza imeunga mkono mpango huu kupitia FCDO ili tuweze kuutekeleza ili kusaidia jamii kuepukana na mabadiliko ya tabia nchi yanayokumba kaunti hizo mbili
Mkurugenzi huyo alidokeza kuwa hatua hiyo inatokana na wito wa katibu mkuu wa umoja wa mataifa António Guterres, wa kutaka ulimwengu kuhamasisha wananchi kuhusu athari za mabadiliko ya tabia nchi.
Alidokeza kuwa wanania ya kupeleka kampeni hiyo katika kaunti nyingine nchini katika siku zijazo.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

