News
Wazee wa Kaya walaumu mgawanyiko wa maandalizi ya Chendachenda
Mungano wa Wazee wa Kaya za Mijikenda umeelezea kusikitishwa na hatua ya serikali ya kaunti ya Kilifi ya kupanga kuandaa tamasha za tamaduni za jamii ya Mijikenda za Chendachenda katika chuo kikuu cha Pwani mbali na maelewano ya kuandaa tamasha hilo kaunti ya Kwale.
Katika taarifa yao kwa vyombo vya habari Muungano huo ulitaja hatua hiyo kama ya kuwakosea heshima Wazee wa Kaya.
Wazee hao walidai kwamba hatua ya serikali ya kaunti ya Kilifi chini ya gavana Gedion Mung’aro inania ya kutenganisha jamii ya Mijikenda mbali na kuwaunganisha.
Aidha walisisitiza kuchukua msimamo na kuandaa tamasha hilo katika Kaya ya Mtswakara kaunti ya Kwale na yeyote atakayeenda kinyume na maamuzi ya Wazee hao atakumbana na laana za wazee.
Waliitaka serikali ya kaunti ya Kilifi kuomba msamaha kutokana na hatua hiyo.

Taarifa ya muungano wa wazee wa Kaya kwa vyombo vya habari
Awali tamasha hiyo iliandaliwa katika kaunti ya Kilifi na ilitarajiwa kuandaliwa katika kaunti tofauti kati ya kaunti sita za Pwani, kulingana na makubaliano ya jamii ya Mijikenda.
Hatua hii imeonekana kusababisha mgawanyiko miongoni mwa viongozi wa Kaya na viongozi wa siasa eneo la Pwani
Taarifa ya Joseph Jira
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

