News
Kundi la MRC lataka Polisi kuwaachilia huru wanachama wake
Kundi la Mombasa Republican Council –MRC limeshinikiza idara ya usalama kuwaachilia huru wanachama wake waliokamatwa.
MRC inadai hatua hiyo inakiuka uamuzi wa Mahakama uliotambua kundi hilo kuwa halali kisheria hivyo kuendelea na harakati zake za kupigania maslahi ya eneo la Pwani.
Viongozi wa kundi hilo wakiongozwa na Msemaji wao Franklin Ngumbao wanadai wanachama wao wamekuwa wakikamatwa, kufuatiliwa na kunyanyaswa kila wanapofanya mikutano ya Amani kuhamasisha umma kuhusu ajenda yao eneo la Pwani.
Serikali ya Kenya inajua vizuri kwamba sisi tulienda Mahakamani na ikatupatia sisi haki kwamba tunaweza kujisimamia wenyewe mambo yetu bila kutatiza serikali ya Kenya, lakini bado makaratasi yako katika hewa tu, ushindi ule haujulikani na serikali ya Kenya.’alisema Ngumbao.
MRC imedokeza kuwa imewasilisha lalama zake kwenye mashirika mbali mbali ya kimataifa yakiwemo umoja wa mataifa, Umoja wa Afrika, Mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa jinai ICC, pamoja na Mahakama ya kimataifa ya haki ICJ ili kupata msaada zaidi.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa kundi hilo Ziro Mwambodza amedokeza kuwa wamekuwa wakifuata njia za kisheria kwa muda japo madai yao hayajaangaziwa.
‘Ilipofika 2016 uamuzi ulitoka kwamba MRC madai yao yako sawa na wanafuata sheria kikamilifu, tumeendelea hivyo kufuata sheria mpaka sasa mahali tumefikia ni kwamba imetulazimu kutafuta msaada katika mashirika ya nje’ alisema Mwambodza.
Taarifa ya Mwanahabari wetu
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

