News
Magavana watishia kususia vikao vya kamati ya seneti kuhusu uhasibu
Baraza la Magavana nchini limetishia kususia vikao vya kamati ya bunge la Seneti kuhusu hesabu za umma, likidai kwamba kumekuwa na vitendo vya uladhalilishaji, ulaghai wa kifedha na unyanyasaji dhidi ya magavana.
Mwenyekiti wa baraza hilo ambaye pia ni Gavana wa Wajir Ahmed Abdillahi, alisema baadhi ya maseneta kwenye kamati hiyo wamekuwa wakiwashambilia magavana kwa kisingizio cha kuuliza maswali pindi wanapofika mbele ya kamati hiyo.
Akisoma taarifa ya pamoja ya magavana hao baada ya kufanya kikao cha mazungumzo mjini Kilifi, magavana walisema hawatahudhuria vikao hivyo hadi masuala tata yatakapotatuliwa kati ya viongozi wa bunge la Seneti na baraza la magavana nchini.
Aidha gavana hao walishikilia kwamba iwapo watalazimika kufika mbele ya makamati mbalimbali za bunge la seneti kuelezea matumizi ya rasilimali za umma basi watafanya hivyo mara moja kwa kila roba ya mwaka.
Katika kikao hiyo Naibu Mwenyekiti wa baraza hilo ambaye pia ni Gavana wa Tharaka Nithi Mothomi Njuki aliwalaumu baadhi ya maseneti kwenye kamati hizo, akisema ndio chanzo cha masaibu hayo.
Taarifa ya Elizabeth Mwende
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

