News
Chacha Mwita, Katwa Kigen na Issack Hassan wateuliwa kuwa majaji wa Mahakama ya rufaa
Rais William Ruto amewateua watu 15 kuwa Majaji wa Mahakama ya rufaa baada ya kuhojiwa na kupigwa msasa na Makamishna wa Tume ya huduma ya Mahakama nchini JSC.
Watu hao wanajumuisha, Jaji wa Mahakama kuu Enock Chacha Mwita, Wakili Katwa Kigen, Johnson Okoth Okello, Lilian Paul, Munyao Sila, Byram Ongaya, Brown Murungi Kairaria, na Stephen Andersen Radido Okiyo.
Wengine ni pamoja na Mwenyekiti wa Mamlaka ya IPOA Ahmed Issack Hassan, Hedwig Imbosa Ong’udi, Mathews Nduma Nderi, Linnet Mumo Ndolo, Lucy Mwihaki Ngujuna, Samson Odhiambo Okongo na Rachel Chepkoech Ngetich.
Katika chapisho la gazeti rasmi la serikali, Rais Ruto kwa kuzingatia kipengele cha Katiba ya 166 ibara ya kwanza (b) kinachompa mamlaka ya kuwateua majaji, Kiongozi wa nchi ametumia kipengele hicho na kutekeleza jukumu lake la kuwateua majaji hao 15.
Hata hivyo baada ya kuapishwa, watahitajika kuanza majukumu yao Mahakamani, wakilenga kuziba pengo la uchache wa Majaji kwenye idara ya Mahakama nchini.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi.
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

