News
Polisi waimarisha doria eneo la Hulugho kufuatia shambulizi la kigaidi
Idara ya usalama nchini imesema imeimarisha doria na operesheni za kiusalama zinaendelea katika kaunti ya Garissa kufuatia shambulio la kigaidi lilitekelezwa katika eneo la Hulugho na kusababisha vifo vya watu wawili.
Idara hiyo ilisema inaendelea kuwasaka waliohusika na mauaji hao, ikisema eneo hilo sasa limedhibitiwa na operesheni za kiusalama zinaendelea kwani maafisa wa usalama wametuma eneo hilo.
Idara hiyo kupitia Inspekta Jenerali wa Polisi nchini Douglas Kanja iliwahakikishia wakaazi wa kaunti hiyo ya Garissa usalama wa hali ya juu na kuwahimiza kudumisha utulivu na kuwa macho.
Hata hivyo baadhi ya walimu wanaohudumu katika shule za kaunti hiyo ikiwemo shule ya msingi ya Hulugho, wameitaka serikali kupitia Tume ya kuajiri walimu nchini TSC kuwapa uhamisho wa haraka ili kuokoa maisha yao.
“Chifu wa eneo hilo na Mwalimu wenzetu walitolewa ndani ya nyumba na kupigwa risasi hadi kuuwawa, na sisi tunaiambia Tume ya TSC itupatie uhamisho, sisi hata hatujui tulale wapi, tuko na wasiwasi kuhusu usalama wake, tunaomba tafadhali serikali tusaidieni jamani”, alisema Mwalimu
Chifu wa eneo hilo, Abdifatah Gani, pamoja na Mwalimu wa Shule ya msingi ya Hulugho, Stephen Musili, ni kati ya waliouawa katika shambulio hilo la usiku wa kuamkia siku ya Jumatatu Januari 26, 2026.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

