Connect with us

News

Mahakama kuu yabatilisha uamuzi wa bunge la Kilifi dhidi ya Spika Mwambire

Published

on

Mahakama kuu ya Malindi imebatilisha uamuzi wa bunge la kaunti ya Kilifi wa kumtimua Mamlakani Spika wa bunge hilo Teddy Mwambire na kuagiza Spika Mwambire kurejea kazini.

Jaji wa Mahakama hiyo J. N Njagi alitoa agizo hilo na kufutilia mbali hatua ya Karani wa bunge hilo Michael Ngala kuchapisha katika gazeti rasmi la serikali la kutangaza nafasi hiyo kuwa wazi hadi kesi hiyo itakaposikiliza na kuamuliwa.

Jaji Njagi aliagiza pia Spika Mwambire kurejea kazi licha ya bunge hilo kumtimua Mamlakani Juni 30 kutokana na madai ya kutokuwa na imani naye.

Jaji Njagi alilitaka bunge hilo kuzingatia kanuni na sheria na kumpa nafasi Spika Mwambire kutekeleza majukumu yake ya kikazi kwa mujibu wa sheria hadi kesi hiyo iliyowasilishwa na Mahakamani itakaposkizwa na kuamuliwa.

Jaji huyo hata hivyo aliwasilisha faili ya kesi hiyo kwa Jaji Mugure Thande ambapo kesi hiyo itaskizwa rasmi mnamo tarehe 14, Julai mwaka huu huku walalamishi wa kesi hiyo akiwemo Kassim Mwadena na Emmanuel Kazungu Chai wakidai kwamba bunge hilo lilikiuka sheria na haki za Spika Mwambire.

Itakumbukwa kwamba mnamo Juni 30 mwaka huu, bunge la kaunti ya Kilifi lilipiga kura 40 kati ya 50 na kuidhinishwa kutimuliwa Mamlakani kwa Spika Mwambire kwa misingi ya ukiukaji wa Katibu, utumizi mbaya wa ofisi ya umma, ukandamizaji wa miradi ya serikali ya kaunti ya Kilifi miongoni mwa shtuma zengine.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending