News
IEBC yahakikishia wakenya usalama wa taarifa za usajali
Tume uchaguzi na mipaka nchini (IEBC) imerejesha tovuti yake ambayo wapigakura huthibitisha taarifa zao za usajili, baada ya kipindi cha ukarabati.
Hii ni kufuatia malalamishi ya umma kuhusu hitilafu isiyoeleweka ambayo ilisababisha mamilioni ya wakenya kushindwa kupata taarifa zao za usajili kama wapigakura.
Tume hiyo ilitangaza kwamba tovuti hiyo sasa imerejea mtandaoni, kufuatia kipindi cha ukarabati wa mfumo unaolenga kuhamisha miundombinu yake ili kuimarisha utendakazi na usalama.
Tangazo hilo lilifuatia siku za sintofahamu ambapo wakenya hawakuweza kuthibitisha maelezo yao ya usajili, iwe kupitia tovuti ya IEBC au kwa njia ya ujumbe mfupi.
Wapigakura walipata ugumu wa kutuma nambari ya kitambulisho au ya pasipoti pamoja na mwaka wao wa kuzaliwa, kulingana na mahitaji ya IEBC.
Njia zote mbili za uthibitishaji hazikuweza kufikiwa wakati wa ukarabati, na hivyo kusababisha wasiwasi kuongezeka, haswa wakati joto la kisiasa linapozidi kuongezeka kuelekea uchaguzi Mkuu wa mwaka 2027.
Katika taarifa iliyotolewa siku ya Jumapili 6, Julai 2025 bodi ya uchaguzi iliwahakikishia wapiga kura, ikisema, “Tungependa kuwahakikishia wakenya wote kwamba maelezo ya usajili wa wapigakura 22,120,458 waliojiandikisha, kama yalivyorekodiwa wakati wa uchaguzi mkuu wa 2022, yanasalia shwari na salama.
IEBC iliongeza kuwa uboreshaji wa mfumo ulikuwa muhimu ili kuimarisha utoaji wa huduma kupitia utendakazi bora wa mfumo na usalama wa data.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

