Connect with us

News

UN yakosoa mauaji ya Saba saba

Published

on

Ofisi ya kamishna mkuu wa haki za kibinadamu wa umoja wa mataifa (OHCHR) imeibua wasiwasi kuhusu maandamano ya siku ya Saba Saba nchini Kenya, ambapo makumi ya raia waliuawa na wengine kujeruhiwa.

Katika taarifa yake siku ya Jumanne, kamishna mkuu wa umoja wa mataifa wa haki za kibinadamu Volker Türk alilaani ukiukwaji wa haki za binadamu nchini Kenya, na kuahidi kushirikiana na Kenya katika kutatua changamoto vile vile katika uchunguzi.

“Tumesikitishwa sana na mauaji ya jana ya takriban watu 10, pamoja na uporaji na uharibifu wa mali nchini Kenya wakati polisi na vikosi vingine vya usalama vilijibu maandamano ya ghasia katika mji mkuu wa Nairobi na kaunti zingine 16. Risasi za sumu, risasi za mpira, gesi ya kutoa machozi na maji ya kuwasha zilitumika,” ilisema OHCHR kupitia msemaji wake Ravina Shamdasani.

Türk alitoa wito wa utulivu pamona na heshima kamili kwa uhuru wa kujieleza, kujumuika na kukusanyika kwa amani.

“Ni muhimu kwamba malalamiko halali katika mzizi wa maandamano haya yashughulikiwe,” alisema.

Kamishna Mkuu pia alihimiza kwamba mauaji na ukiukwaji wa haki za binadamu “kuchunguzwa kwa haraka, kikamilifu, kwa uhuru na kwa uwazi.”

Wakati wa maandamano ya Julai 7, 2025, polisi waliripoti kwamba raia 11 waliuawa na 567 walikamatwa.

Pia, huduma ya kitaifa ya polisi (NPS) ilisema maafisa 52 na raia 11 walijeruhiwa, magari 12 ya polisi, magari 3 ya serikali na magari 4 ya raia yaliharibiwa.

“Chini ya sheria ya kimataifa ya haki za binadamu, nguvu ya kimakusudi ya maafisa wa kutekeleza sheria, ikiwa ni pamoja na silaha, inapaswa kutumika tu inapobidi ili kulinda maisha kutokana na tishio linalokaribia,” aliongeza Türk.

Maandamano yaliyoshuhudiwa siku ya Saba Saba yalikuja baada ya wiki mbili tu baada ya raia 15 kuuawa mnamo Juni 25, 2025.

Kisha, wakenya waliandamana katika ukumbusho wa mauaji ya zaidi ya watu 60 wakati wa maandamano ya kupinga ushuru mnamo Juni 2024.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending