Connect with us

News

Mahakama Kuu yasitisha mpango wa Marekani na Kenya wa Karantini

Published

on

Mahakama Kuu nchini imesitisha kwa muda mpango wa serikali ya Marekani na Kenya wa kuanzisha kituo cha karantini cha Ebola humu nchini.

Jaji wa Mahakama hiyo, Patricia Nyaundi, ameagiza kusitishwa kwa muda kwa utekelezaji wa makubaliano hayo hadi pale kesi iliyowasilishwa Mahakamani itakaposikilizwa na kuamuliwa.

Katika uamuzi wake, Jaji Nyaundi alisema Kenya pia hairuhusiwi kupokea mtu yeyote aliyekumbana na Ebola au aliyeambukizwa ugonjwa huo chini ya mpango huo hadi kesi hiyo itakapomalizika.

Shirika la kutetea haki za kiraia la Katiba Institute liliwasilisha kesi hiyo mahakamani likipinga mpango huo siku hiyo hiyo ulipotangazwa.

Shirika hilo limesema kuanzishwa kwa kituo hicho kwa siri na bila ushirikishwaji wa umma kunazua maswali mengi kuhusu haki za maisha, afya, uwajibikaji wa serikali na usimamizi wa bunge.

Kabla ya kesi hiyo kuwasilishwa Mahakamani, Serikali ya Marekani kupitia Rais Donald Trump ilikuwa imekubaliana na Kenya na kutangaza mpango wa kuwahifadhi kwa muda raia wake waliokumbana na virusi vya Ebola nchini Kenya.

Hatua hii ililenga kuzuia ugonjwa huo kuingia katika ardhi ya Marekani, ambapo sasa mpango huo umekumbana na kikwazo kikubwa baada ya Mahakama kuu nchini kusimamisha kwa muda mpango huo.

Kwa mujibu wa Ikulu ya White House, raia wa Marekani waliokuwa katika maeneo yenye mlipuko wa Ebola lakini hawajaonyesha dalili za ugonjwa huo walitarajiwa kuwekwa katika kituo maalum cha karantini katika Kambi ya Anga ya Laikipia mjini Nanyuki.

Maafisa wa utawala wa Marekani walikuwa wamesema wale ambao wangepata dalili za Ebola hawangerejeshwa Marekani, bali wangepelekwa katika nchi nyingine kwa matibabu ya juu zaidi.

Hatua hiyo ilionekana kuwa mabadiliko makubwa ya sera ikilinganishwa na milipuko ya Ebola iliyopita ambapo wagonjwa Wamarekani waliruhusiwa kurejeshwa nyumbani kwa matibabu.

Lengo la mpango huo lilikuwa kuhakikisha hakuna kisa cha Ebola kinachoingia nchini Marekani.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Ukataji wa miti kaunti ya Kilifi wakashifiwa

Published

on

By

Wadau mbalimbali wa mazingira katika kaunti ya Kilifi waliungana katika chuo kikuu cha pwani kuadhimisha siku ya mazingira ulimwenguni, hafla ambayo ilianza na zoezi la upanzi wa miche elfu 5.

Katika hafla ambayo iliongozwa na mkurugenzi wa mazingira kaunti ya Kilifi, Jimmy Yaa walisema licha ya taifa kuwekeza katika matumizi ya kawi safi na upanzi wa miche, bado juhudi zaidi zinapaswa kuwekwa kukabiliana na changamoto za kimazingira zinazotatiza harakati hizo.

Kwa upande wa Ruwa Kalama kutoka idara ya misitu kaunti ya Kilifi alisisitiza haja ya Wananchi kupanda miche ya matunda na kuwaonya wakaazi dhidi ya kukata miti kiholela ili kukabiliana na madailiko ya hali ya anga.

“Kadri tunavyopanda miche, tusisahau kupanda ile ya matunda na pia kaunti ya Kilifi ni Kati ya zile kaunti ambazo zinakata miti kihole”, alisema Kalama

Naye Kamanda wa Polisi eneo la Kilifi Kaskazini, kaunti ya Kilifi Stanley Tanui, alisema idara ya usalama imekuwa katika mstari wa mbele kuhakikisha sheria ambazo zinawekwa kudhibiti uchafuzi wa mazingira zinatekelezwa vilivyo.

“Kama idara ya usalama Kilifi Kaskazini, hata sisi tunahusika pakubwa katika uhifadhi wa mazingira na kuhakikisha sheria za kudhibiti uchafuzi wa mazingira zinatekelezwa vilivyo” alisema Tanui

Maadhimisho haya yalilenga kuhamasisha jamii kuchukua hatua madhubuti za kupunguza athari za uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya hali ya anga kote ulimwenguni.

Kauli mbiu ya mwaka huu ni “Kuchukua hatua dhidi ya mabadiliko ya hali ya hewa”

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Mahakama ya Kilifi yawatupa gerezani washtakiwa zaidi ya 10

Published

on

By

Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa washtakiwa zaidi ya 10 waliowasilishwa Mahakamani wakikabiliwa na mashtaka mbalimbali ikiwemo kesi za unajisi na makosa ya jinai.

Katika vikao vya Mahakama siku ya Jumatano tarehe 3 June 2026, Hakimu Ivy Wasike ametoa hukumu hizo kwa watuhumiwa hao huku wengine wakifungwa kwa zaidi ya miaka 30 gerezani.

Simon Ngala, Aliwali Ali Mwalimu, Christopher Buru, miongoni mwa wengine zaidi ya 10 walifikishwa katika Mahakama ya Kilifi na kuhukumiwa kufuatia mashtaka mbalimbali yanayowakabili ikiwemo mashtaka ya unajisi na makosa ya jinai.

Hakimu wa Mahakama ya Kilifi Ivy Wasike, alimhukumu kifungo cha miaka 30 gerezani Simon Ngala baada ya kupatikana na hatia ya kumnajisi mtoto wa miaka 13 kisha akamtorosha kwao kwa kipindi cha mwezi mzima.

Mwengine ni Aliwali Ali Mwalimu, aliyehukumiwa kifungo cha miaka 25 kufuatia mashtaka ya kumpachika ujauzito mtoto wa miaka 13 licha ya kuomba msamaha Mahakamani.

Wakati wa kutoa hukumu hizo, Hakimu Wasike alisikitishwa na kukithiri kwa visa vya watoto kupotea na kisha kunajisiwa katika kaunti ya Kilifi.

Kiongozi wa mashtaka katika Mahakama hiyo Nancy Njeru alipinga vikali ombi lililowasilishwa Mahakama la kutaka washtakiwa wasamehewe, kwanin wengine walidai kwamba walishirika makosa hayo bila kukusudia, akisema hukumu hizo zitakuwa funzo kwa watu wenye hulka hizo katika jamii.

Mbali na hukumu za kesi za unajisi, Christopher Buru alihukumiwa kifungo cha miaka miwili gerezani akikabiliwa na mashtaka ya wizi baada ya kupatikana na hatia ya kutumia pesa za mlalamishi Saumu Nyevu aliyekuwa akimtumia pesa alipokuwa akifanya kazi katika milki za kiarabu, kosa lililomchukiza zaidi Hakimu Wasike.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading

Trending