News
Mahakama ya mnyima dhamana mshukiwa wa Mihadarati
Mahakama ya Kilifi imeagiza mshtakiwa wa kesi ya usafirishaji wa Mihadarati aina ya bangi kuendelea kuzuiliwa rumande wakati kesi hiyo ikiendelea.
Akitoa agizo hilo Hakimu wa Mahakama hiyo Charles Obulutsa alisema kuwa mshtakiwa anafaa kurudishwa mahakamani mnamo tarehe 19 mwezi Septemba mwaka huu.
Kabla ya agizo hilo kutolewa Mahakama ilielezwa kwamba mnamo tarehe 7 mwezi Agosti mwaka 2024, maafisa kutoka kituo cha polisi cha Kilifi wakiwa katika ziara ya usalama walikamata gari lililokuwa limeegeshwa kando ya barabara mjini Kilifi lenye nambari ya usajili KCF 259K aina ya Subaru likiwa limebeba gunia saba za bangi huku dereva wa gari hilo asijulikane aliko.
Kulingani na maelezo ya afisa mchunguzi wa kesi hiyo gari hilo lilipelekwa hadi kituo cha polisi cha Kilifi ambapo mwenye gari ambaye ni Ezra Omondi alijitokeza baadaye na kueleza kwamba alikuwa amelikodisha gari hilo kwa mshtakiwa Reagan Onyango Otieno.

Bangi ya thamani ya mamilioni ya pesa yanaswa mjini Kilifi
Mahakama pia ilielezwa kwamba maafisa wa polisi waliweza kumkamata mshtakiwa mnamo tarehe 7 mwezi Oktoba mwaka 2024 baada ya mwenye gari kueleza kwamba mshukiwa alikuwa ametorokea katika kijiji cha Dago kaunti ya Kisumu na kisha baadaye kusafirishwa hadi mjini Kilifi katika kituo cha polisi cha Kilifi mnamo tarehe 8 mwezi Oktoba mwaka 2024 na hatimaye kufunguliwa mashtaka.
Mahakama pia ilimnyima dhamana mshukiwa Reagan Onyango Otieno baada ya kusakwa na maafisa wa upelelezi kwa mda mrefu.
Kesi hiyo itaendelea mnamo tarehe 19 mwezi Septemba mwaka huu.
Taarifa ya Teclar Yeri
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

