News
Maiti tano zafukuliwa eneo la Kwa Binzaro kaunti ya Kilifi
Maiti tano zimefukuliwa kutoka eneo la kwa Binzaro kaunti ya Kilifi, siku ya kwanza ya zoezi la kufukua maiti eneo hilo.
Maafisa wa upelelezi wanaohusika na mauaji kutoka idara ya DCI wamefukua makaburi 6 ambapo vipande 10 zaidi vya miili ya binadam viliepatikana.
Zoezi hilo la kufikua maiti lilifanywa kufuatia idhini ya idara ya mahakama huku maafisa wa upelelezi wakitarajiwa kuendelea kufukua makaburi 21 zaidi katika eneo hilo.
Mwanapatholojia wa serikali Daktari Richard Njoroge alitoa wito kwa wanafamilia ambao huenda walipoteza wapendwa wao kufika katika hospitali ya Malindi ambapo sampuli za DNA zitachukuliwa na kufanyiwa vipimo.
Naye afisa wa masuala ya dharura katika shirika la kutetea haki za binadam la Haki Afrika- Mathius Shipeta alidokeza kuwa safari hii miili ilikuwa imefichwa tofauti na ilivyoshuhudiwa katika msitu wa Shakahola.
Zoezi la ufukuaji maiti linatarajiwa kuendelea Ijumaa 22, Agosti 2025, huku ikihofiwa huenda kuna watu zaidi walizikwa katika eneo hilo la Kwa Binzaro.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

