News
Makubaliano ya UDA na ODM
Mkutano wa wabunge wa bunge la kitaifa na Seneti wa Chama ODM na UDA kuhusu utekelezaji wa mchakato wa ajenda 10 zilizoidhinishwa kati ya Rais William Ruto na Hayati Raila Odinga mwezi Machi mwaka 2025, umefanyika.
Hatua hii inayonyesha utofati wa misimamo ya kisiasa kati ya viongozi wa ODM huku Seneta wa Nairobi Edwin Sifuna, Gavana wa Siaya James Orengo, Mbuge wa Embakasi mashariki Babu Owino wanaopinga ushirikiano ODM na UDA, wakikwepa mkutano huo.
Mwenyeti wa Kamati ya utekelezaji wa mchakato wa ajenda 10, Dkt Agnes Zani wakati wa mkutano huo uliyoandaliwa katika ukumbi wa KICC jijini Nairobi, alielezea mafanikio ya ajenda 10, akisema mchakato huo hauna mipaka na utaendelea kutekelezwa hadi matakwa ya wakenya yaafikiwe.
Gavana wa Kisumu Prof Anyang’ Nyong’ aliye mwanachama wa ODM, alisisitiza haja ya suala la ugatuzi kutekelezwa kikamilifu sawa na mgao wa serikali hizo kusambazwakwa wakati huku Kiongozi wa wachache bungeni Junet Mohamed akimkumbusha rais Ruto kuhusu deni la shilingi bilioni 12 ambalo chama cha ODM kinadai serikali.
Kinara wa Chama cha ODM Dkt Oburu Oginga alisisitiza kwamba mpango wa serikali jumuishi utaendelea hadi mwaka 2027 pamoja na mchakato wa ajenda 10 kutekelezwa, huku akiitaka serikali kuweka kitengo cha kukabiliana na majanga.
Hata hiyo Rais William Ruto alisema uwajibikaji ni lazima kwa kila kiongozi na mchakato wa ajenda 10 utatekelezwa zaidi huku akihimiza viongozi kujitolea kupambana na ufisadi, akisisitiza huduma zote za kiserikali kupitia mfumo wa kidigitali.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

