News
Viongozi wa UDA kaunti ya Kilifi wafanya mkutano kuangazia mikakati ya Chama mashinani
Viongozi wa Chama tawala cha UDA kaunti ya Kilifi wamekutana kuangazia mipango na mikakati ya kuimarisha chama hicho mashinani.
Kati ya masuala yaliyojadiliwa ni pamoja na viongozi hao kufanya kazi pamoja na jamii katika ngazi ya mashinani ili kuendeleza maendeleo, uongozi jumuishi na dhamira ya kujenga mustakabali imara kwa mwananchi.
Katika kikao hicho kilichoongozwa na Naibu Kiongozi wa wengi bungeni ambaye pia ni Mbunge wa Kilifi Kazkazini Owen Baya, viongozi hao waliangazia pia suala la kuendeleza malengo ya chama cha UDA mashinani pamoja na kusajili wafuasi wapya.
Viongozi hao pia waliahidi kuweka kando tofauti zao za kisiasa na kushirikiana, kwa lengo la kuhakikisha kaunti ya Kilifi inanufaika kimaendeleo kutoka kwa serikali kuu.

Viongozi wa Chama tawala cha UDA kaunti ya Kilifi wafanya mkutano wa kuimarisha chama mashinani
Viongozi waliohudhuria kikao hicho ni pamoja na Mwenyekiti wa bodi ya barabara nchini Aisha Jumwa, Mwenyekiti wa bodi ya hazina ya michezo, vijana na Sanaa Wakili George Kithi, Mbunge wa Ganze Kenneth Kazungu Tungule miongoni mwa viongozi wengine, ambao ni wafuasi wa chama cha UDA.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

