Connect with us

News

Mashahidi wafichua maovu kwenye kesi ya Shakahola

Published

on

Ushahidi wa kutisha umeendelea kufichuliwa katika kesi ya mauaji ya Shakahola, ambapo Mhubiri tata Paul Mackenzie na washukiwa wenzake 35 wanakabiliwa na mashtaka mazito ikiwemo ukatili wa watoto, mateso, na unyimwaji wa elimu.

Kesi hiyo iliendelea kusikilizwa mbele ya Hakimu mkuu Nelly Chepchirchir katika Mahakama ya Watoto ya Tononoka kaunti ya Mombasa huku mashahidi wanne wakitoa ushahidi wao.

Mmoja wa mashahidi, Maxwell Kisienya, ambaye ni Mkurugenzi wa shule ya Bridge International Academy Lungalunga, alieleza kuhusu mwanafunzi aliyetoweka baada ya kuondolewa shuleni kwa kushindwa kulipa karo mnamo tarehe 19 Oktoba 2017 na tokea hapo, shule haikupokea maombi yoyote ya uhamisho, wala hakujulikana alipoelekea mwanafunzi huyo.

Katika ushahidi wa kidijitali, Koplo Joseph Mwai, mtaalamu wa uchunguzi wa kidijitali kutoka Kitengo cha Kupambana na Ugaidi, ameeleza mahakama jinsi alivyovuna taarifa kutoka kwa simu ya shahidi ambapo aligundua picha nne za watu waliokonda kupita kiasi.

Aidha, mtaalamu wa upasuaji wa maiti, Dkt. Richard Njoroge, alithibitisha kwamba miili mingi kati ya ile 453 iliyofukuliwa kutoka makaburi ya halaiki ilikuwa katika hali ya kuharibika kupita kiasi huku akieleza kwamba katika baadhi ya miili, njaa kali ndiyo iliyotajwa kuwa chanzo cha kifo kutokana na ukosefu mkubwa wa uzito wa mwili.

Kwa mujibu wa daktari huyo, sampuli za meno, mifupa na kucha zilichukuliwa kutoka kwa miili hiyo na kufanyiwa vipimo vya DNA, ambapo baadhi ya waathiriwa sasa wametambuliwa kupitia familia zao.

Mahakama pia ilisikiliza ushahidi kutoka kwa Inspekta mkuu Job Wafula Wanyonyi, aliyekuwa miongoni mwa kikosi cha kwanza kilichofika Shakahola kufuatia ripoti za kijasusi, mnamo tarehe 13 mwezi Aprili 2023, ambapo aliwaokoa watu waliokuwa wakiishi kwenye vibanda duni, wengi wao wakiwa dhaifu kiasi cha kushindwa hata kuzungumza.

Aliongeza kuwa baadhi ya watu waliokamatwa walikuwa wakilinda maeneo hayo wakiwa na silaha kama rungu na jembe.

Kesi hiyo itaendelea kusikilizwa siku Jumatano, Septemba 17 mwaka huu.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending