Connect with us

News

Mashirika ya kupigania amani Kenya yang’aa kwenye tuzo Tanzania

Published

on

Mashirika ya Kenya ya kupigania amani katika jamii yameendelea kujizolea sifa na umaarufu katika taifa jirani la Tanzania baada ya kutuzwa kwenye mashindano ya mpango wa “Amani na Usalama- (IPSA)” mwaka 2025 yaliyoandaliwa jijini Dar es Salaam, Tanzania.

Miongoni mwa mashirika yaliyotuzwa ni shirika la Re-Imagining New Communities ambalo limetuzwa kutokana na mchango wake wa kupigania mageuzi ya amani kupitia elimu ya amani na ushirikiano wa dini mbalimbali unaolenga watoto, walimu na wachungaji nchini Kenya.

Akipokea tuzo kwa niaba ya shirika hilo, Grace Wendo msimamizi wa mipango katika shirika hilo, alielezea ushindi huo kama “uthibitisho wa athari ambazo shirika limekuwa nazo tangu kuanzishwa kwake 2021.

“Nishani hii ni ya kila mtoto ambaye ameongoza mazungumzo katika maabara yetu ya amani, kila mwalimu ambaye amefanikisha mazingira ya darasa salama na la malezi, kila kiongozi wa kidini ambaye ametetea umoja, na kila jumuiya ambayo imechagua maridhiano badala ya migawanyiko”,  alisema Bi Wendo.

Shirika la Re-Imagining New Communities limekuwa nguvu inayoongoza katika ujumuishaji wa ujenzi wa amani Kenya.

Mtazamo wake unaozingatia mtoto huwapa vijana uwezo wa kuwa mawakala wa mabadiliko, wakati programu zake za kiimani na mazungumzo ya jamii hutengeneza majukwaa salama ya kushughulikia mizozo na kukuza mshikamano wa kijamii.

Bi Wendo alisisitiza kuwa utambuzi huo ni ukumbusho kuwa amani haijengwi na mtu mmoja mmoja, bali ushirikiano wa jamii.

Utambuzi huo unakuja katika wakati muhimu huku Jumuiya kote Afrika Mashariki zikiendelea kukabiliana na masuala ya migogoro, ubaguzi na ukosefu wa usalama.

Kwa kutwaa tuzo hiyo, Re-Imagining New Communities iliiweka Kenya mstari wa mbele katika juhudi za amani na usalama zinazoendeshwa mashinani, na hivyo kuimarisha mchango wa nchi katika ajenda pana ya amani ya Afrika.

“Huu sio mwisho wa safari yetu,” aliongeza Bi Wendo. “Ni wito wa kwenda mbali zaidi, kufikia jamii zaidi, na kuhakikisha kuwa amani inashikiliwa na kila mtoto na kila familia.”

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending