Connect with us

News

Mashirika ya kupigania amani Kenya yang’aa kwenye tuzo Tanzania

Published

on

Mashirika ya Kenya ya kupigania amani katika jamii yameendelea kujizolea sifa na umaarufu katika taifa jirani la Tanzania baada ya kutuzwa kwenye mashindano ya mpango wa “Amani na Usalama- (IPSA)” mwaka 2025 yaliyoandaliwa jijini Dar es Salaam, Tanzania.

Miongoni mwa mashirika yaliyotuzwa ni shirika la Re-Imagining New Communities ambalo limetuzwa kutokana na mchango wake wa kupigania mageuzi ya amani kupitia elimu ya amani na ushirikiano wa dini mbalimbali unaolenga watoto, walimu na wachungaji nchini Kenya.

Akipokea tuzo kwa niaba ya shirika hilo, Grace Wendo msimamizi wa mipango katika shirika hilo, alielezea ushindi huo kama “uthibitisho wa athari ambazo shirika limekuwa nazo tangu kuanzishwa kwake 2021.

“Nishani hii ni ya kila mtoto ambaye ameongoza mazungumzo katika maabara yetu ya amani, kila mwalimu ambaye amefanikisha mazingira ya darasa salama na la malezi, kila kiongozi wa kidini ambaye ametetea umoja, na kila jumuiya ambayo imechagua maridhiano badala ya migawanyiko”,  alisema Bi Wendo.

Shirika la Re-Imagining New Communities limekuwa nguvu inayoongoza katika ujumuishaji wa ujenzi wa amani Kenya.

Mtazamo wake unaozingatia mtoto huwapa vijana uwezo wa kuwa mawakala wa mabadiliko, wakati programu zake za kiimani na mazungumzo ya jamii hutengeneza majukwaa salama ya kushughulikia mizozo na kukuza mshikamano wa kijamii.

Bi Wendo alisisitiza kuwa utambuzi huo ni ukumbusho kuwa amani haijengwi na mtu mmoja mmoja, bali ushirikiano wa jamii.

Utambuzi huo unakuja katika wakati muhimu huku Jumuiya kote Afrika Mashariki zikiendelea kukabiliana na masuala ya migogoro, ubaguzi na ukosefu wa usalama.

Kwa kutwaa tuzo hiyo, Re-Imagining New Communities iliiweka Kenya mstari wa mbele katika juhudi za amani na usalama zinazoendeshwa mashinani, na hivyo kuimarisha mchango wa nchi katika ajenda pana ya amani ya Afrika.

“Huu sio mwisho wa safari yetu,” aliongeza Bi Wendo. “Ni wito wa kwenda mbali zaidi, kufikia jamii zaidi, na kuhakikisha kuwa amani inashikiliwa na kila mtoto na kila familia.”

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending