News
Miili 7 zaidi yagunduliwa Kwa Binzaro na kufikisha idadi ya miili 32
Shughuli ya kufukuaji wa maiti katika vichaka vya Kwa Binzaro eneo la Shakahola kaunti ndogo ya Magarini inaingia wiki ya pili huku miili 7 zaidi ikifukuliwa Alhamisi Agosti 28.
Kupatikana kwa miili hiyo sasa inafikisha idadi ya maiti zilizofukuliwa katika kijiji Kwa Binzaro kuwa watu 32 waliofariki katika awamu ya pili ya sakata ya mauaji ya kinyama eneo la Shakahola.
Maafisa wa serikali wa uchunguzi wa maiti wakiongozwa na Daktari Richard Njoroge, walisema miili hiyo iliharibika kiasi cha kutombulika huku wakipata vipande vingine 54 vya miili vikiwa vikitapakaa katika eneo la tukio.
Hii inaaminika kwamba baadhi ya miili hiyo ililiwa na wanyamapori kwani ilikuwa imezikwa katika makaburi ya kina kifupi sana.
Sakata hii ya Shakahola 2 inazidisha hofu hasa miongoni mwa wakaazi wa sehemu hiyo ya Shakahola kukiwa na taarifa kwamba huenda baadhi ya miili hiyo ilisafirisha hadi eneo hilo la Kwa Binzaro.
Mapema mwezi uliopita maafisa wa usalama, kwa ushirikiano na wenyeji walifumania kundi la watu wanaoaminika kwamba ni wafuasi wa itikadi kali katika msitu huo wa Kwa Binzaro ambao baadhi yao walifanikiwa kutoroka.
Maafisa wa Polisi waliwazuilia korokoroni watu sita kuhusiana na sakata hiyo ya Kwa Binzaro, ambayo imetokea miaka michache tu tangu kisa cha kwanza na shakaola One chini ya uongozi wa Mhubiri tata Paul Mackenzie.
Waumini wa Kanisa la Mhubiri Mackenzie waaminika walilazimishwa kufunga hadi kufa kwa imani kwamba watakutana na Yesu.
Mackenzi na wenzake wako korokoroni wakisubiri uamuzi wa Mahakama kuhsu kesi ya mauaji inayowakanili.
Taarifa ya Eric Ponda
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

