Connect with us

News

Mwalimu wa Madrasa adaiwa kumlawiti mvulana eneo la Kwa Mwango mjini Kilifi

Published

on

Hali ya wasiwasi na ghasia zilishuhudiwa katika eneo la Kwa Mwango karibu na Mkoroshoni mjini Kilifi Agosti 28, 2025.

Hii ni baada ya wakaazi wenye hasira kuvamia madrassa ya msikiti wa Masjid Rehema, wakipinga tuhuma za udhalilishaji wa watoto unaofanywa na Mwalimu wa Madrasa hiyo.

Kulingana na walioshuhudia tukio hilo walisema kisa hicho kilidhiirika wakati mama mmoja alipofichua kwamba mwanawe ambaye ni mwanafunzi wa madrasa hiyo kwamba alilawitiwa na mwalimu mmoja wa madrasa hiyo.

Mama huyo ambaye alikuwa akipiga nduru na kulalamikia madhila aliyofanyiwa mwanawe yalisababisha umati wa watu kuvamia madrassa hiyo na bweni la wanafunzi hao, wakitaka kuchoma majengo ya madrassa hiyo kwenye msikiti huyo wa Masjid Rehema.

Wakaazi hao walivamia msikiti huo wakiwa na dhamira ya kumuadhibu Mhubiri huyo huku wengine wakifunga barabara ya Kilifi – Malindi pamoja na kuwasha moto, hali iliyosababisha msingamano wa magari katika eneo hilo ambalo kwa kawaida huwa na shughuli nyingi.

Wenyeji hao walivunja lango na kuingia msikitini na kuanza kumshanbulia Mhubiri huyo ambaya baadaye aliokolewa na Maafisa wa usalama ambao walimkamata mshukiwa na kumpeleka kituo cha Polisi mjini Kilifi.

Maafisa wa Polisi wamnusuru Mwalimu wa madrassa ya msikiti wa Masjid Rehema

Maafisa hao wa usalama wameeleza vyanzo vya habari Kwamba wanaendelea na Uchunguzi na mshukiwa atafikishwa mahakani hivi karibuni.

Taarofa ya Eric Ponda

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending