Connect with us

News

Mkurugenzi wa KPA Kapteni William anusurika kwenye ajali ya barabarani

Published

on

Afisa mkuu mtendaji wa Mamlaka ya Bandari nchini (KPA) Kapteni William Ruto, amenusurika baada ya kuhusika kwa ajali mbaya ya barabarani iliyosababisha kifo cha binti yake, huku wanafamilia wengine wakinusurika na kupokea matibabu.

Katika taarifa iliyotolewa na Mamlaka ya KPA ilisema ajali hiyo ilitokea siku ya Ijumaa jioni alipokuwa akisafiri pamoja na familia yake, na kuthibitisha kuwa binti yake alifariki dunia huku wengine wakinusurika katika ajali hiyo.

Mamlaka hiyo ilieleza kuwa Kapteni Ruto na familia yake wako katika hali thabiti na chini ya uangalizi wa karibu wa madaktari, na ikaeleza matumaini ya kupona kwa haraka na kikamilifu kutokana na majeraha waliyopata.

“Tunasikitika sana kwa msiba huu mzito na tunatoa pole zetu za dhati kwa Kapteni Ruto na familia yake katika kipindi hiki kigumu,” ilisema Idara ya Mawasiliano ya KPA.

Mamlaka hiyo iliomba familia hiyo ipewe faragha wakati huu wa maombolezo, ikiwahimiza umma na vyombo vya habari kuheshimu nafasi yao wanapokabiliana na msiba huo.

Ilitambua msaada kutoka kwa Gavana wa Mombasa Abdulswamad Shariff Nassir na Gavana wa Taita Taveta Andrew Mwadime kwa msaada wao wa haraka kufuatia ajali hiyo.

Idara hiyo pia iliwashukuru wafanyakazi, washirika, wadau na umma kwa msaada wao, uvumilivu na ushirikiano wao wakati wa tukio hilo na mchakato wa kupona.

KPA ilisema inaendelea kushirikiana na mashirika husika kubaini chanzo na mazingira ya ajali hiyo na itatoa taarifa zaidi kadri maelezo zaidi yatakavyopatikana.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending