News
Mswada wa marekebisho ya Katiba wa mwaka 2026 umewasilishwa bungeni
Mswada wa marekebisho ya Katiba wa mwaka 2026 na sheria za uchaguzi umewasilishwa katika bunge la Seneti.
Mswada huo unalenga kufanyia marekebisho kipengele cha Katiba cha 99 na 193 pamoja na sheria za uchaguzi sehemu ya 24 na 25 ili kuwepo na uwazi kwa magavana wanaolenga kuwania nyadhfa za uongozi baada ya kukamilisha mihula yao.
Mswada huo uliowasilishwa na Seneta wa Kirinyaga James Murango unalenga pia kuzuia magavana waliomaliza mihula yao ya uongozi kutowania nyadhfa za useneta, ubunge ama uwakilishi wadi, kwani inakuwa vingumu kuchunguzwa.
Kuwasilishwa kwa mswada huo bungeni kufuatia hali magavana kuwania wadhfa wa useneta baada ya kukamilisha mihula yao ya uongozi hali ambayo imeleta sintofahamu ya kiuongozi, ikiashiria tamaa za uongozi na njama ya kuhitilafiana na ufuatiliaji wa matumizi ya raslimali za umma.
Seneta Murango alisema katika utekelezaji wa majukumu yao, magavana hulazimika kuwajibika mbele ya mabunge ya kaunti na Seneti kuhusu matumizi ya kifedha na kiutawala.
Wakati huo huo alidokeza kwamba iwapo mswada huo utapishwa na kuwa sheria utasaidia kufutilia usimamizi wa raslimali za kaunti na matumizi ya fedha kwani utazuia magavana kuhitilafiana na uchunguzi.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

